• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Dumisheni Nidhamu Muendelee Kuwa wa Kwanza Mkoani Kagera: Bahama

Wakati ilipowekwa: April 3rd, 2019

Wanajamii wa shule ya sekondari ya Lukole katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, wametakiwa kudumisha nidhamu, ili waendelee kushika nafasi ya kwanza katika shule za sekondari mkoani Kagera, kwenye mthani wa kidato cha sita mwaka 2019.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wiulaya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama, ameyasema hayo Machi 29, 2019 wakati akikabidhi cheti cha pongezi kwa uongozi wa shule hiyo wakati wa Mahafali ya sita, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brig. Jen. Marco Elisha Gaguti.

“Tulikusanya vyeti vinne, ambapo shule zangu zote zilifanya vizuri, lakini Lukole sekondari ikiwa ya kwanza; tafsiri yake ni kwamba shule ya Lukole ina nidhamu, kwa sababu mahali penye nidhamu, ushirikiano na umoja ndipo matunda mazuri yanatoka.” Alisema Ndugu Bahama.

Kwa hiyo, ufaulu huu ni matokea ya uwepo wa nidhamu shuleni, nishamu ya walimu, nidhamu ya wanafunzi na nidhamu ya wafanyakazi wasio walimu, kwa sababu mtoto ambaye hana nidhamu hana nafasi kwenye shule zetu.

Amesema vijana 342 wasichana 116 na wavulana 226 wameweza kuhitimu masomo yao, kwa sababu ya kuwa na nidhamu, huku akidai kuwa shule ya sekondari Lukole ni sehemu sahihi ya wanafunzi kujifunza kulingana na jiografia, na umahili wa walimu wao.

“Hatutegemei kwamba sifa ya ufaulu tuliyonayo, ambapo kwa kipindi cha miaka sita tumefaulisha kwa 100%, kwamba mwaka huu itapungua; ni matumaini yangu kwamba wanafunzi hawa watafaulu kwa 100%, lakini kwa kuanzia daraja la I na II.” Alisema Bahama.

hata hivyo, amewapongeza wazazi kwa malezi yao yaliyotukuka ya kitanzania na hatimaye kuwawezesha kuifikia siku ya leo, ambapo watoto wao wanahitimu masomo yao; huku akidai kwamba, mzazi mwenye nidhamu uzaa na kulea watoto wenye nidhamu.

Risala ya wanafunzi pamoja na mambo mengine waliomba wapewe kompyuta ili ziwasaidie katika kujifunza, Mkurugenzi Mtendaji aliahidi kuwaongezea kopmpyuta pindi atakapowiwa, maana Tumaini Fund walikuwa wamewapatia kompyuta tayari.

“Hata siku moja mtu binafsi hawezi kumiliki ardhi ya shule” hilo ni tamko la Waziri wa Ardhi, na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi alilotamka alipokuwa Wilayani Ngara mwaka 2018, Ndugu Bahama alikariri tamko hilo, kuonyesha makosa ya baadhi ya wananchi, wanaojitwalia ardhi za shule kwa nguvu.

Amesema hawezi kumpa haki mtu mmoja na kuwaacha 600, wakiwa hawana mahali pa kujenga miundombinu ya shule, huku akiahidi kuwatuma maafisa ardhi, wafanye tathimini na ikigundulika mwananchi huyo ana haki ya kumiliki ardhi hiyo, atampatia ardhi nyingine.

“Niwaombe mvute subira wakati tukiangalia jinsi ya kutatua changamoto hizi; kwa mfano, hapa naona upungufu wa nyumba za watumishi, mimi pamoja na watendaji wenzangu katika Halmashauri tutajipanga tuweze kufanya mikakati ya kukabiliana na changamoto hizo.” alisema Ndugu Bahama.

Aidha, ametoa wito kwa wazazi kutoa ushirikaino wa kuziwezesha shule hizo pindi watakapotakiwa kufanya hivyo kwa madai kwamba shule za sekondari hususani hizi za kidato cha tano na cha sita, zinamilikiwa na wazazi na Halamshauri kama serikali.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa