• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Hatutaki Mwanafunzi Abaki Mwaka 2020 Kwa Sababu ya Ukosefu wa Miundombinu

Wakati ilipowekwa: January 16th, 2019

“Wanangara tulione suala la kuchangia huduma ya elimu ni letu, mwaka 2020 hatutaki mwanafunzi abaki, kwa sababu ya ukosefu wa miundombinu ya darasa.” Alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wialya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama.

Ndugu Bahama amesema wananchi wanachangishana na wanachokipata kinapelekwa kwenye ujenzi wa miundombinu shuleni, kwani kila kijiji kina shule kama siyo ya sekondari basi kitakuwa kinamiliki shule ya msingi, hivyo lazima waandae miundombinu ya shule zote.

“Na kuchangia siyo hiari ni lazima; kwa hiyo kwa mwaka huu, tutachangia tu; kwa kazi au kwa fedha, kwa ajili ya kukamilisha vyumba vya madarasa 128 vya shule za msingi, lakini na vyumba vya madarasa 48 katika shule za sekondari.” Alisema Bahama.

Halmashauri pamoja na wafanyakazi wake wamechangia takribani shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mashueni, ambapo Halmashauri imechangia shilingi milioni 24, huku wafanyakazi wote wakichangia milioni 25; Mkurugenzi shilingi 50,000/= wakuu wa idara na vitengo shilingi 20,000 kila mmoja, wafanyakazi shilingi 10,000 pamoja na wahudumu shilingi 5,000/=.

Amesema shule zote wanaeendelea na ujenzi, na kudai kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Ngara haikuwa na upungufu mkubwa; wanahamasisha wananchi wajenge vyumba vya madarasa vinavyopungua mwaka huu; wakilenga upungufu wa madarasa ya wanafunzi watakaoingia mwaka 2020.

Amezitaja madarasa saba yaliyopungua kwamba yanajengwa katika shule za Nyakisasa, Rusumo ‘B’, Kanazi, Mugoma, pamoja na Mabawe, ambapo hata hivyo mapungufu ni kidogo, “lakini tunashukuru kote mambo yanakwenda vizuri.” Alisema Ndugu Bahama.

“Katika maandalizi ya vyumba vya madarasa; sisi tuko vizuri kwa sababu tunatakiwa kujenga madarasa saba, lakini katika ziara niliyoifanya ya Januari 13, 2019 nimekuta vyumba vingi viko kwenye renta na tunatarajia mwezi ujao kama tarehe 15, 2019 vyumba hivyo viwe vimekamilika.” Alisema Ndugu Bahama.

Halmashauri kwa sasa inahamasisha kila kijiji kiwe na benki ya tofali 300,000 kwani tafali laki tatu mara vijiji sabini na mbili itakuwa tofali za kutosha, kukomesha tatizo la upungufu wa miundombinu mashuleni.

Kapeini hiyo, itazinduliwa rasmi Machi 30, 2019 ili kupisha kwanza ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa ajili ya wanafunzi wanaotakiwa kujiunga na masomo yao ifikapo Machi 15, 2019; baada ya hapo itaanza kujenga madarasa mengine ya kupokea wanafunzi wa mwaka 2020.

Baadhi ya vijiji vimekwishaanza kujenga vyumba vya madarasa kwa ajili ya kupokea wanafunzi watakaoingia awali, darasa la kwanza pamoja na wa kidato cha kwanza mwaka 2020, ambazo amesitaja kuwa ni shule ya Kibimba inaendelea na ujenzi wa madarasa 02 yamefikia renta.

Shele nyingine ni Rusumo ‘B’ darasa moja linakaribia kwenye renta, ambapo shule nyingine za msingi na za sekondari nao wanaendelea na ujenzi wa miundombinu hiyo; huku akisema kwamba shule za sekondari wanaupunfu wa vyumba 48, lakini vinavyojengwa 34 kwa hiyo upunfu madarasa 14.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • MAJALIWA AZINDUA MITAMBO YA SHILINGI BILIONI 12.4 KWA AJILI YA WACHIMBAJI WADOGO

    June 26, 2025
  • MAONESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA YAFANYIKA KITAIFA DODOMA

    June 17, 2025
  • RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AFANYA UFUNGUZI WA DARAJA LA J.P MAGUFULI (KIGONGO - BUSISI)

    June 19, 2025
  • KAGERA YAINGIA ROBO FAINALI MICHEZO YA UMITASHUMTA

    June 15, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa