• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Imarisheni Uongozi wa Vikundi Kabla ya Kuomba Mikopo

Wakati ilipowekwa: May 10th, 2019

Wanufaika wa mfuko wa akinamama, vijana na walemavu katika Halmashauri ya wilaya ya Ngara, wametakiwa kuimarisha uongozi wa vikundi na kuinua kipato chao, kabla ya kuomba fedhaya mkopo toka katika mfuko huo.

Wito huo umetolewa na wanakikundi mbalimbali, waliotembelewa na idara ya Maendeleo ya Jamii Wilayani Nagra, ili kujiridhisha na uwepo wa vikundi vilivyoomba mkopo, kabla ya kutoa fedha kwa vikundi hivyo, Mei 08, 2019 katika kata za Rusumo, Nyakisasa, Rulenge na Kabanga.

“Wanakikundi wengi wanashindwa kurejesha mikopo waliochukua, kwani uongozi usiokuwa imara, unashindwa kuwaimiza wanakikundi, kurejesha mikopo yao kwa wakati ikizingatiwa kuwa maisha ya wanakikundi hao ni duni.” Alisema Ndugu Audax Alex mwanakikundi cha Rusumo Bodaboda Group.

Ndugu Alex amesema kutokurejesha fedha ya mkopo kwa wakati maana wanamaanisha kwamba viongozi wao watiwe hatiani, kwani kila mmoja anajua kwamba fedha ya mkopo siyo zawadi lazima irejeshwe kwa wakati, ili vikundi vingine.

Naye Valerian Audax amefafanua kwamba kikundi chao cha Bodaboda Group kimefanikiwa kurejesha fedha yote waliokopa kwa wakati kwa sababu ya kuwa na uongozi thabiti, huku kila mmoja akitimiza wajibu wake kwa kuhakikisha fedha hiyo imeufikia huogozi wao kwa wakati muafaka.

Akieleza jinsi walivyonufaika na mkopo wa akinamama, vijana na walemavu, Ndugu Audax amesema fedha waliyopata imewasaidia kukuza kipato chao kwani kutegemema bodaboda pekee haitoshi, kwani wakati wa mvua hawapati wateja wa kutosha, lakini kwakuzungusha fedha hiyo wameinua maisha yao.

“Tulitumia fedha hiyo kama mtaji wa kipato cha ziada, baada ya kupata hiyo fedha nilimpatia mke wangu ambaye aliitumia kuuza mboga na samaki; kwa kweli imenisaidia kwani wakati huu wa mvua hatupati wateja wa kutosha katika shughulizaetu za bodaboda.” Alisema ndugu Audax.

Bi. Juliana Tumaini wa kikundi cha Umoja ni Nguvu wa kijiji cha Kashinga katika kata ya Nyakisasa, amewashauri wanavikundi katika Wilaya ya Ngara kutumia mikopo wanayopokea katika malengo waliyoeleza wakati wa kupata mkopo, kwani wengi wamekuwa wakikiuka malengo yao na kufanya kinyume.

Aidha, Bi. Tumaini amesema wao, wamefanikiwa kurejesha fedha hiyo, kwa sababu wameitumia katika malengo waliyojiwekea na kuelewana; na kuongeza kwamba kuelewana huko kunaondoa tofauti zao.

Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Bi. Avelina Kabyazi, amewashukuru wanakikundi waliorejesha fedha hiyo kwa wakati, na kuwasistiza kuepuka udanganyifu aliosema umeshamiri miongoni mwa wanakikundi wengi.

“Kutorejesha fedha hiyo kwa wakati ni kujizuilia faida wenyewe; kwani mtafungiwa kupewa mikopo, mtaawakwamisha wanavikundi wengine kupata mkopo kwa sababu fedha, ambayo ingezunguka kwa wanavikundi hao, inakuwa mikononi mwa wachache wasiokuwa waaminifu. Alisema Bi. Kabyazi.

Halmashauri ya Wilaya ya Ngara imekuwa ikitenga asilimia 10 kila mwezi, kutoka katika mapato yake ya ndani, kwa ajili ya kutoa mikopo kwa akinamama, vijana na walemavu, katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NGARA YAFANYA VIZURI MICHEZO YA SHULE ZA MSINGI UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA

    May 30, 2025
  • MHE. COL MATHIAS KAHABI DC NGARA AKUTANA NA BALOZI WA RWANDA.

    May 29, 2025
  • NGARA YAENDELEA VIZURI NA MICHEZO YA SHULE ZA MSINGI UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA.

    May 26, 2025
  • MADEREVA WAPATIWA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI ILI KUPUNGUZA AJALI - NGARA

    May 24, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa