• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Jitokezeni Mpate Elimu Ya Utalii Mkuze Kipato Chenu; DED Ngara

Wakati ilipowekwa: April 30th, 2019

 Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara wametakiwa kujitokeza kwa wingi, wapate elimu katika sekta ya utalii, ili waweze kuinua kipato chao, lakini na serikali iweze kupata mapato yake.

Hayo ni Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama ofisini kwake April 30, 2019, kwamba Halmashauri ina dhamana ya kuwaandaa wananchi wake, ili waweze kuingia katika uchumi huo wa kitalii.

 “Wilaya ya Ngara inakwenda kuingia katika biashara ya kitalii, lakini katika uwekezaji nimeona ni busara Halmashauri ya Wilaya ya Ngara ina vijana, ambao wanaweza kufanyakazi katika eneo hili la utalii, nimeona niwaandae kwa fursa hiyo, wasiweje kuwa wasindikizaji.” Amesema Ndugu bahama.

Kwa sasa ninaandaa Halmashauri imeandaa programu, ambayo itakuwa kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Ngara na vyuo vya kitalii vya Musoma Utalii College kilichoko Tabora na Arusha Utalii College kilichoko Arusha kwa lengo la kuwaandaa wananchi, kutumia fursa inayoletwa na hifadhi ya Burigi.

Katika kufanikisha azma hiyo, amewasiliana na Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Kagera ambaye ameridhia na kukubariana na wazo hilo, na kuongeza kwamba tayari wamefanya mazungumzo ya awali na vyuo hivyo, ambayo watayakamilisha mwezi Mei 2019.

“Mipango itakapokamilika vitakuwa na dhamana ya kuja kuwafundisha wananchi wetu hapa wilayani Ngara, kwa sababu natambua watu wengi hawana uwezo wa kwenda kusoma kwenye vyuo hivyo, na wenye uwezo hawana muda wa kwenda vyuoni.” Amesema Ndugu Bahama.

Kwa matakwa ya Mkurugenzi huyo Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ay Ngara, wananchi waanze kusoma kazi fupi fupi, zitakazo wawezesha kuufahamu utalii, lakini kuwandaa kuingia katika soko la utalii

Kwa upande wa wafanyabiashara anapendekeza wawe na elimu ya jinsi ya kujenga hoteli, kambi za kupokelea watalii na vituo vya habari na mawasiliano, huku akiwataka vijana kujifunza kozi za Hotel Management, Hospitality, Tour guards pamoja na potters, wakiyajua watapata ajira.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Erick Nkilamachumu, amesema kwamba hifadhi ya Burigi kuwa mbuga za wanyama, itapelekea kukua kwa uchumi wa wilaya zinazozunguka Mbuga hiyo.

Amezitaja Wilaya hizo kuwa ni Ngara, Biharamulo, Muleba na Karagwe; ma kwamba ni matumaini yao kwamba katika siku za usoni uchumi wa wana Ngara utapanda, huku akiwataka wananchi kujipanga kutumia fursa hiyo kwa kuandaa mazingira mazuri.

Pamoja na hayo, amewakumbusha wananchi, wajiadae kwa kuongeza uzalishaji ikiwa ni pamoja na kulima mazao ya chakula nay a biashara kwa ajili ya wageni watakaoitembelea Wilaya ya Ngara.

“Siyo wakulima tu, bali hata wafanyabisahara, wataweza kuongeza kipato chao kwa kuuza vitu vyao, lakini kinachotakiwa ni wafanyabisahara hao kujipanga, ili wahakikisha bidhaa zote muhimu, zinapatikana na katika ubora unaotakiwa.” Alisema Nkilamachumu.

Diwani wa Kata ya Murusagamba Wilaya Ngarani Ndugu Soud Mukubira amesema kwamba suala la utalii katika wilaya ya ngara ni fursa kwa wananchi hasa vijana wao, ambao watapata mafunzo, na hatimaye inawezekana wakapata ajira.

“Kwetu sisi, hiyo ni fursa kwa sababu utalii umekuwa katika wilaya na mikoa ya mbali, lakini kwa sasa tumepata nafasi ya kuingia katika mzunguko wa utalii; kwa hiyo tutaweza kutembelea mbuga hizo ndani ya wilaya ya yetu.” Alisema Ndugu Mkubira.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NGARA YAFANYA VIZURI MICHEZO YA SHULE ZA MSINGI UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA

    May 30, 2025
  • MHE. COL MATHIAS KAHABI DC NGARA AKUTANA NA BALOZI WA RWANDA.

    May 29, 2025
  • NGARA YAENDELEA VIZURI NA MICHEZO YA SHULE ZA MSINGI UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA.

    May 26, 2025
  • MADEREVA WAPATIWA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI ILI KUPUNGUZA AJALI - NGARA

    May 24, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa