• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Ishini Malengo ya Mwenyezi Mungu Waleeni Watoto Kiimani na Kimaadili

Wakati ilipowekwa: May 21st, 2019

Waumini wa madhehebu yote hapa nchini, wametakiwa kuishi kadiri ya utaratibu na malengo ya Mwenyezi Mungu, unaowataka mume na mke kusaidiana, kuzaa pamoja na kuitawala dunia, huku wakiwalea watoto wao, katika maadili yanakubalika kidini na kijamii.

Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge-Ngara Mhashamu Sevelin Niwemugizi, ameyasema hayo ofisini kwake Mei 17, 2019; kwamba wanafamilia wamemweka Mwenyezi Mungu pembeni, matokeo yake jamii inakata tama na kukosa mwelekeo.

Baba Askofu Niwemugizi anaamini kwamba suala la familia kuwa na imani na maadili yaliyotukuka, haliwahusu waumini wa dhehebu fulani tu, bali ni suala la kijamii zaidi; akidai kwamba kama jamii ipo, ni kwa sababu kuna ndoa na vitu vya msingi vinavyoigusa.

 “Ikishafikia mahali wanafamilia wakamweka Mwenyezi Mungu pembeni, wakamuweka nje ya mipango/utaratibu wa maisha yao, ndiyo mwisho wa familia hiyo. lazima wanafamilia wamshukuru na kumwomba Mungu awabariki.” Amesema Askofu Niwemugizi.

Baba Askofu anasema lengo la kwanza la wanandoa ni kusaidiana kama Maandiko Matakatifu yanavyosema, mume na mke wasaidiane, wazae na waongezeke; lakini Mwenyezi Mungu akawapa kazi nyingine ya kuitawala dunia. “Sasa tujiuliza katika jamii ya leo haya malengo watu wanayaishi?”

Kinyume na malengo ya Mwenyezi Mungu Baba Askofu Niwemugizi, anasema kwamba watu wanaoana kwa malengo tofauti; mwingine anataka mtu wa kumzalia mtoto tu, mwingine anataka mali na mwingine anataka msomi, na kuongeza kwamba ndoa ni zaidi ya hayo, ndiyo maana jamii imetunga sheria ya ndoa.

Katika kuzaa kuna wajibu wa kulea, ambayo ni pamoja na kuelimisha, kutia maadili mema, nidhamu na kuwaelekeza watoto katika imani, wazazi kama walivyofunuliwa na Mwenyezi Mungu, imewapasa kuwavuvia maadili mema watoto wao, ili wawe raia wema, na waumini wanaoishi kadiri ya maelekezo ya Mwenyezi Mungu.

“Lakini nasikitika kwamba mambo hayako hivyo; watu wanaingia kwenye ndoa kwa malengo yao au kwa miunganiko ya ajabu tunayoisikia; mimi nasema, tukitaka kwenda sawa; lazima jamii irudi nyuma iangalie mpango wa Mwenyezi Mungu kwetu sisi ni upi? Je huu mpango tunauheshimu na kuishi?” Aliuliza Askofu Niwemugizi.

Amesema mtu anaamuka asubuhi anaondoka kwenda kutafuta fedha, lakini anasahau kumtanguliza Mwenyezi Mungu, anayemwezesha kutafuta fedha/mali, hivyo akawashauri wamtangulize Mwenyezi Mungu, ili awabariki kwa kuwapatia watoto waadilifu na mali.

Aidha, amewataka wanafamilia kuwa na utulivu wa ndani; akimaanisha kila mwanafamilia, apate muda wa kutafakari na kujitazama; ametoka wapi, yuko wapi na anakwenda wapi; na kudai kwamba hiyo ni sifa muhimu kwa wanafamilia.

Amewahimiza wanafamilia wanapokabiliana na changamoto wajiweke mbele ya Mwenyezi Mungu na kumwambia tatizo lao, ili aweze kuwaonyesha njia ya kuyashinda yanayowakwaza na kuwapeleka kusikofaa.

Tabia mbaya zinazoonekana katika jamii zetu, chanzo chake ni familia; akitoa mfano ametaja mihemko, unyanyasaji, wivu, mauaji, ukatili, ubakaji/ulawiti na hata ushirikina vinaanzia kwenye familia; ambavyo amevitaja kuwa ni matokeo ya familia zisizomtanguliza Mwenyezi Mungu.

“Kama ni nidhamu tunayoiona sehemu zetu za kazi, shuleni na kwingineko, vinaanzia kwenye familia, ndiyo maana tukitaka kurekebisha mambo, kuwa na utulivu na amani, lazima tuanzie kwenye familia.” Alisema Baba Askofu Niwemugizi.

Kufuatia jamii kubadilika; Baraza la Maaskofu Katoliki la Tanzania, limeamua kuwaongoza waamini wake, kuwambudu Mwenyezi Mungu kuanzia ngazi ya familia, kwenye jumuia ndogo ndogo na kisha kwenye Ibada ya Misa takatifu kila Jumapili.

“Sisi Maaskofu Katoliki Tanzania, tuliwaomba waumini wetu wakati wa Kwaresima, watafakali juu ya familia kama kanisa la nyumbani, na shule ya imani na maadili; wakitumaini kwamba waamini wakirithishana imani yao, na wakajikabidhi kwa Mungu; watakuwa imara, na familia zao zitabaki salama.” Alisema Mhashamu Niwemugizi.

Mwenyezi Mungu, aliwaumba mke na mume, ili wazae na waongezeke, na kwa mpango huo, tunapata tunda la ndoa ambalo ni familia, inayowajumuisha Baba na Mama na baadae watoto; ambapo maandiko matakatifu yanasema “tumeumba vitu vyote, lakini hatujaumba kitu kinachofanana nasi.”

“Mungu anasema tufanye mtu kwa mfano wetu na sura yetu, alipomuumba Adamu akalifika mahali akasema, lakini huyu mtu ataishije peke yake!! Lazima huyu awe na msaidizi wake, akamtengeneza mwanamke akasema, huyo atakuwa msaidizi wake.” Alisema Askofu Niwemugizi.

Aidha, kadiri ya Baba Askofu huyo, ndoa ni muungano kati ya mume na mke, lakini kunyume na hekima na Busara ya Mwenyezi Mungu; changamoto mbalimbali katika jamii zinasababisha waumini wakiuke makusudi ya Mwenyezi Mungu, ambapo leo hii Mwanaume na Mwanaume wanaoana.

Katika jamii yetu imepita Sunami (Utandawazi) na kuwaacha wanafamilia, wakishangaa na kulalamikia kuvunjika kwa maadili, Baba Askofu anaiona familia kama mti wa matumaini, ambao lazima ulishwe mbolea, ili baadae utoe mbegu zilizo njema.

Aidha, mmonyoko wa maadili katika jamii, umepelekea Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, kutafuta mbinu mbadala ya kuwafunda vijana, wanaotaka kumtumikia mwenyezi Mungu kama mapadre, ili waweze kuitambua jamii walimotoka na wawe tayari kuisaidia wakishapadrishwa.

“Sisi hatutoki kwenye kisiwa, tunatoka kwenye familia zetu, zilizokwishaathirika na yanayoendelea, kwa mfano, kutojali imani, na baadhi ya wazazi hawasali kabisa; hilo tumeliona na tunajua kwamba ni changamoto kubwa sana.” Alisema Baba askofu Niwemugizi.

 Amesema tofauti na zamani vijana wengi, walipokuwa wakifundshwa maadili mema wakiwa seminari ndogo, siku hizi wanapata changamoto ya kupata vijana wengi kutoka shule za kata, kwa hiyo, wanahitaji kufanyakazi ya ziada, kuwaandaa vijana hao, kwa ajili ya kazi hiyo muhimu.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa