• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Kagera Yatembelewa na Maafisa Kutoka Nchi 11 na Wanafunzi 16 wa Chuo cha Ulinzi cha Taifa

Wakati ilipowekwa: January 11th, 2019

Ujumbe wa Kitaifa wa Maafisa wa Vyombo Mbalimbali vya Ulinzi na Usalama kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (National Defence Collage) ukiwakilisha nchi 11 wameutembelea Mkoa wa Kagera kujifunza na kubadilishana ujuzi katika masuala ya Ulinzi na Usalama.

Ujumbe huo umefanya mafunzo hayo mkoani Kagera Januari 7, 2019, ambapo pamoja na kubadilishana ujuzi na uongozi wa Mkoa katika masuala ya Ulinzi na Usalama, wametumia fursa hiyo kushauriana njia stahiki za kukuza uchumi Mkoani humo.


Maafisa 16 kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa ukiwa na Maafisa kutoka nchi za Tanzania, Kenya, Nigeria na China mara baada ya kuwasili Mkoani Kagera, ulipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti ofisini kwake.

Akieleza lengo la safari yao, Kiongozi wa Ujumbe huo Balozi Peter Kallage, alisema wamekuja kuja Mkoani Kagera, kujifunza na kubadilisha mawazo katika Nyanja za ulinzi na usalama kimataifa na kuona namna bora ya kuendeleza fursa mbalimbali za kukuza uchumi mkoani humo.

“Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) kipo chini ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na kinaendesha kozi mbali mbali za Kimataifa kama unavyoona; hapa tuna Maafisa kutoka nchi nne kama nilivyozitaja hapo awali, lakini kwa kozi hii, ambayo imetuleta hapa Kagera ina Maafisa kutoka nchi 11 na tumewagawanyika katika makundi 04, weninge wamekwenda katika mikoa mingine sisi tumechagua kuja Kagera.” Alifafanua Balozi PETER KALLAGE

Ujumbe huo kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa ulipitishwa kwenye Wasifu wa Mkoa wa Kagera wa Kiuchumi na Kijamii, ili kuonesha maendeleo ya Mkoa, Fursa mbalimbali za uwekezaji na changamoto katika kukuza uchumi wake na uchumi wa wananchi kwa ujumla.

Katika wasilisho hilo Mkuu wa Mkoa Gaguti, alisema kuwa pamoja na Mkoa wa Kagera kufanya vizuri kiuchumi; lakini changamoto kubwa ni Wahamaiaji Haramu, na Biashara ya magendo ya Mazao.

“Pamoja na Mkoa wetu kuwa na fursa nzuri za kiuchumi kwa kupakana na nchi tatu za Rwanda, Burundi na Uganda na kuwa kitovu cha biashara cha Jumuiya ya Afrika Mashariki; lakini bado tunakabiliwa na changamoto ya Wahamiaji haramu na Biashara ya Magendo ya mazao. lakini tunapambana nao.” Alieleza Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Amesema kwamba pamoja na changamoto hizo wanaendelea kushirikiana na viongozi wenzao wa nchi jirani kukomesha uhamiaji haramu, pia uongozi wa Mkoa umeanzisha Mkakati wa Nyumba Kumi bora ukilenga kukomesha biashara hiyo.

Maafisa hao mara baada ya kupitishwa kwenye Wasifu wa Mkoa walishauri namna ya kuimarisha Ulinzi na Usalaama katika Mkoa, na namna bora za kuzitumia fursa za kiuchumi zilizopo katika Mkoa wa Kagera, ili kuinua uchumi wa mkoa huo na kuchangia pato la Taifa.

Kiongozi wa ujumbe huo aliushukuru Uongozi wa Mkoa wa Kagera kwa kukubali ombi la chuo hicho, kuuleta ujumbe wa Maafisa hao Mkoani Kagera, kujifunza fursa mbalimbali za Kiuchumi, kiulinzi na kiusalama na kuona fursa za uwekezaeji zilizomo Mkoani humo.

Aidha, ujumbe wa Maafisa 16 kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa utakuwepo Mkoani Kagera siku saba, kwa ajili ya kutembelea maeneo mbalimbali ya uwekezaji, utalii, viwanda na kujionea shughuli mbalimbali za uzalishaji mali Mkoani Kagera.

Na: Sylvester Raphael

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa