• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Huwezi Kusimamia Taaluma Rejesha Barua ya Uteuzi; REO Kagera

Wakati ilipowekwa: April 16th, 2019

“Haki ya Mungu ninawaambia; kama uliteuliwa Afisaelimu kata au Mkuu wa shule kwa lengo la kupumuzika na siyo kusimamia taaluma, urejeshe barua ya uteuzi wako, maana unaondoka muda si mrefu.” Alisema Afisaelimu wa Mkoa wa Kagera Ndugu Alyce Kamamba.

Ndugu Kamamba ametoa rai hiyo, akiongea na Mafisaelimu, wakuu wa shule, walimu wa Taaluma wa shule za sekondari na za msingi mwezi April 2019, kwamba viongozi katika sekta ya elimu, imewapasa kusimamia majukumu yao, ili kuinua taaluma mkaoani humo.

“Ukicheza na nyani unakula mabuha, maafisaelimu mkicheza naanza na ninyi; watumieni walimu mlionao kuinua taaluma mkoani Kagera, na anzeni kuwachuje wazembe kwa kuangalia shule za mwisho katika matokeo.”  Alisema Ndugu Kamamba.

Amesema kwa mujibu wa nafasi mbalimbali katika sekta ya elimu, kila mwaajiriwa ana majukumu yake, lakini baadhi yao hawatimizi wajibu wao inavyotakiwa, Akitoa mfano, amesema kuna baadhi ya wakuu wa shule kazi yao ni kuzunguka na cheki tu huku kazi vituoni kwao zikilala.

Msimamizi huyo wa Elimu Mkaoni Kagera, ameagiza kila shule iwe na kamati ya taaluma, ambayo itamsaidia mkuu wa shule, kupitia maswali ya mitihani, ili kuona kama ni ya viwango vinavyokubalika.

Pia, amewataka kuanzisha ‘clubs’ za masomo na za mazingira, shuleni na kuwataka kuzitumia kikamilifu, ili kuboresha taaluma na mazingira ya shule, ikiwa ni pamoja na kupanda miti ya matunda na ya vivuli.

Mkoa wa Kagera mwaka 2019 umejipanga kutopoteza mtoto, kwa hiyo watoto walioandikishwa kujiunga shule ya sekondari au ya msingi, lazima wamalize masomo yao ya darasa la VII, na wa sekondari lazima wamalize kidato cha IV au cha VI, kwa ufaulu wa 100%.

“Ili tuhakikishe kwamba tunaondoa daraja la IV na 0, nimeelekezwa na mkoa ifikapo tarehe Augost 30, 2019, kila mwalimu awe amemaliza mada zake tunaanza marudio; ukibaki na mtoto ambaye amefeli huyo ni wa kwako, na utajua pa kumpeleka.” Alisema Ndugu Kamamba.

Amwaagiza maafisaelimu, kuhakikisha mkoa unafaulisha wanafunzi kwa asilimia zote, na hakuna mtoto hata mmoja anayepotea, na kuwataka wawatumie walimu waliona kwani walimu wa masomo ya sanaa wapo wa kutosha, shida ni ya walimu wa masomo ya sayansi.

Kuhusu watoro, ameagiza walimu wakuu kupitia bodi na kamati za shule kutumia sheria ya elimu, kwamba mtoto akikosa shule kwa siku 90, kama alikuwa mgonjwa anapewa barua ya kukariri, na kama ni mtoro aondolewe kwa mujibu wa sheria iliyopo.

“kwa hiyo wewe mkuu wa shule kazi yako ni kuwasiliana na vyombo vya serikali kudhibiti utoro, mtoro amethibitika aonekani shuleni, tunamuondoa kwa mujibu wa sheria iliyopo.” Alisema ndugu Kamamba.

Kikaokazi hicho kinafuatia ratiba aliyojipangia Afisaelimu Mkoa ya kuwahamasisha walimu katika ufundishaji na ujifunzaji, huku akiwapongeza kwa kazi nzuri ya kuadibisha, na kuwafundisha watoto wa taifa hili.

“Nilianza na Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, na baadae nikaja Halmashauri ya wilaya ya Karagwe, nako nimefanyakazi kwa siku kadhaa, leo niko Halmashauri ya wilaya ya Ngara, baada ya hapa nitaendelea na Halmashauri zilizobaki.” Alisema Msimamizi huyo wa Elimu Mkaoni Kagera.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa