• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Msibadili Usanifu wa Miradi Fuateni Ushauri na Taratibu: Ngombalemwiru

Wakati ilipowekwa: March 27th, 2019

Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) Mh. Vedastus Edger Ngombalemwiru ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, kuacha tabia ya kubadili usanifu wa miradi bila kufuata ushauri na taratibu zilizopo.

Mh. Ngombalemwiru amesema haya wakati wa majumuisho baada ya kamati hiyo, kutemebelea miradi ya Maji ya Munjebwe na Mbuba Machi 26, 2019, iliyoanza kujengwa mwaka 2013 hadi 2019 kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 813.

“Baada ya kukagua miradi ya maji ya Munjebwe na Mbuba, tumabaini kwamba kulikuwa na udhaifu katika kutekeleza miradi hii, hali iliyopelekea mradi wa Munjebwe kujengwa chini ya kiwango.” Alisema Mh. Ngombalemwiru.

Kadiri ya Mwenyekiti huyo, kulikuwa na marekebisho yaliyofanywa katika mikataba bila kufuata taratibu zilizopo, na kuiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Ngara kuwakilisha nyaraka za mabadiliko hayo kwa CAG, ifikapo Juni 01, 2019 kwa ajili ya kuyafanyia uhakiki.

Wameiagiza Halmashauri hiyo, kuhakikisha mapungu yote ya mradi wa maji wa Munjebwe, yamerekebishwa kwa kutumia ‘detention money’ kama Mhandisi na Mkurugenzi, walivyoahidi na taarifa ya utekelezaji huo, iwasilishwe kwa CAG na kamati hiyo kabla ya tarehe 01/06/2019.

Aidha, wameagiza mwanasheria wa RAS, ashirikiane na Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, kuhakikisha kwamba doasari za kisheria zilizojitokeza zinarekebishwa na makubaliano ya sasa yanakuwepo kisheria; ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza baadae.

Pia, wameitaka ofisi ya Mkuu wa Mkoa na TAMISEMI, kuhakikisha Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, inapata mwanasheria, atakayetoa ushauri wa kitaalamu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa.

Kadiri ya Mhadisi wa Idara ya Maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Eng. Simon Ndyamukama, mradi wa maji wa Munjebwe ulianza kutekelezwa mwaka 2013 kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 287.

Akijibu maswali ya wanakamati, Eng. Ndyamukama amekiri kwamba mradi huo haujawanufaisha wananchi kutokana na mapungufu yaliyojitokeza katika mradi huo, ikiwemo kuvuja kwa tenki na kupelekea baadhi ya wananchi walengwa wa mradi huo kutopata maji kama ilivyokusudiwa.

Eng. Ndyamukama ameiambia kamati kwamba kutokana na mapungufu hayo, mradi bado uko mikononi mwa mkandarasi hadi marekebisho hayo yatakapo fanyiwa kazi, na wananchi wakapata huduma ya maji kadili ya makusudi ya serikali.

Wananchi wa Kijiji cha Munjebwe wamethibitisha kuwa maji wanayopata kutokana na mradi huo, yanakuwa ni kidogo ikilinganishwa na mahitaji halisi ya wananchi hao.

Akisoma taarifa ya mradi wa maji wa Mbuba, Eng. Ndyamukama, amesema kwamba mradi huo ulianza kujengwa mwaka 2014 kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 524, lakini hadi sasa haujakamilika kwa sababu ya serikali kuchelewesha fedha ya kulipa madai ya mkandarasi.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Erick Nkilamachumu, ameiomba Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, kuishauri serikali kuleta fedha za miradi ya maendeleo kwa wakati, ili miradi hiyo ikamilishwe kwa wakati.

“Kwa sababu ninyi mko Bungeni naomba muishauri serikali, watuletee fedha kwa wakati kwa ajili ya miradi inayotekelezwa huku vijijini; kwa sababu haingii akilini kwamba miradi ya maji ya mwaka 2013 hadi 2019 bado haijakamilika.” Alisema Ndugu Nkilamachumu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama, ameiambia kamati hiyo, kwamba watahakikisha ushauri uliotolewa na kamati hiyo, unafanyiwa kazi, ili miradi iwe na tija kwa wananchi.

Ndugu Bahama ameishukuru kamati hiyo kwa kuichagua Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, kwani mapendekezo yanayotolewa, yanalenga kuleta ufanisi wa miradi ya maendeleo kwa manufaa ya mlengwa, ambaye mwananchi.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa