• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Msiwasajiri Wahamiaji Haramu Katika Taasisi Zetu za Elimu

Wakati ilipowekwa: November 29th, 2018

“Msiwasajiri wahamiaji haramu katika taasisi zetu za elimu, bali muwaelekeze katika ofisi zetu za uhamiaji, ili tuwape vibali vya kusoma hapa nchi, tusipofanya hivyo tunaandaa mawaziri na viongozi wasio raia wa Tanzania.” Alisema Mkaguzi wa Uhamiaji Wilayani Ngara Ndugu Said Ali Malengo.

Ndugu Malengo ametoa rai hiyo, wakati wa Kikao cha Ushauri cha Wilaya, kilichofanyika Novemba 28, katika ukumbi wa Halmashauri chini ya uenyekiti wa mkuu wa Wilaya hiyo Lt. Col. Michael Mntenjele.

Tatizo la wahamiaji kusoma katika tasisi za elimu hapa nchini, linasababishwa na viongozi katika mashina wasiokuwa wazalendo, kwa sababu wanapotaka kwenda shule wanapewa barua ya kupata cheti cha kuzaliwa na viongozi hao.

Wahamiaji haramu si raia wa Tanzania wanaposoma katika taasisi za elimu hapa nchini wanatumia gharama kubwa za taifa, ambazo kihalali si haki yao na haziwahusu, hivyo wanazikosa watanzania, ambao kimsingi ndio wenye haki nazo.

Mme aliyemuoa mke mhamiaji anatakiwa kuripoti ofisi ya uhamiaji, ili apate kibali cha ukaazi ambacho atakilipia shilingi 100,000 au dola 50, na akiwa na watoto watakapofikia umri wa kwenda shule atapewa kibali bure cha kuwaruhusu watoto hao kusoma hapa nchini.

Lengo la kumpatia kibali hicho, ni kumkumbusha kwamba yeye si mtanzania ni mhamiaji, kwa hiyo, hata akisoma kwa kiwango gani tayari, atakuwa na rekodi inayomuonesha kwamba yeye si raia wa Tanzania, bali ni mhamiaji.

Amekikumbusha kikao hicho, kwamba raia wa kigeni anapoingia hapa nchini, lazima awe na viza na ikiwa ni mwanachama wa nchi za Afrika Mashariki, atapata visa ya matembezi aliyoiita ‘Holyday visa’ bila malipo yoyote.

Mhamiaji anapokuwa na visa ya matembezi haruhusiwi kuhusika kwa namna yoyote ile katika shughuli ya kiuchumi, na ikiwa mwenyeji wake, anataka kumtumia itabidi aende ofisi ya uhamiaji, amlipie dola 100 itayodumu kwa muda wa miezi mitatu, kinyume chake atalipa faini ya dola 600 au kifungo.

Aidha, amesema ili kuepuka hilo, wanapokamata wahamiaji haramu wanakamata aliyehamia na aliyemleta hapa nchini; “sisi na polisi ni wamoja tunapofanya operation tunawakamati wahamiaji na wamiliki wa wahamiaji hao.” Alisema Ndugu Malengo.

Kwa sababu wakiachwa wamiliki wa wahamiaji haramu, matokeo yake wamiliki wa wahamiaji hao, wanawakaribisha tena; kwa hiyo, dawa ni kuwakamata wote; wahamiaji na wamiliki wao.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa