• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

RAIS DKT SAMIA ANATAMBUA MCHANGO WA MADHEHEBU YA DINI KATIKA KUENDELEZA MAARIFA - MAJALIWA

Wakati ilipowekwa: September 20th, 2025

Asema elimu haiwezi kukamilika kama hakuna maadili.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua kwa dhati mchango wa madhehebu ya dini ikiwemo BAKWATA na wadau wote wa elimu katika kuimarisha maadili, kuendeleza maarifa na kuleta mshikamano wa kitaifa kupitia elimu.

Amesema kuwa elimu haiwezi kukamilika kama hakuna maadili kwani ndiyo yanayojenga utu, heshima na mshikamano wa kijamii. "Serikali ya Awamu ya Sita imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha elimu inakuza maarifa na ujuzi, sambamba na malezi yanayoimarisha tabia bora na maadili ya kizalendo kwa vijana wa Kitanzania".

Amesema hayo Jumamosi Septemba 20, 2025 alipomwakilisha Rais Dkt. Samia katika hafla ya usiku ya utoaji tuzo za elimu za mufti iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Serena hotel jijini Dar es Salaam.

"Rais Dkt. Samia anawapongeza sana BAKWATA kwa juhudi kubwa mnazozifanya katika masuala yote ya maendeleo ya jamii hususan mchango wenu katika kuendeleza elimu na kuimarisha mshikamano wa kitaifa kupitia malezi ya maadili na maarifa, Serikali inathamini sana mchango wa taasisi za dini kama BAKWATA katika kuunga mkono malezi ya watoto na vijana". Amesema Mheshimiwa Majaliwa.

Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) limekuwa na mchango mkubwa katika kukuza sekta ya elimu nchini kwani limeanzisha na kuendesha shule, madrasa na vyuo vinavyotoa elimu bora ya dini na ya kawaida, sambamba na kujenga maadili mema kwa vijana.

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Tuzo za Elimu za Mufti ni jukwaa la kitaifa la kutambua na kuthamini michango ya kipekee katika elimu, ubunifu, malezi na maadili ya vijana wa Kitanzania. "Tukio hili linaakisi muonekano wa taifa lenye watu wanaojituma, wanaothamini elimu, na wanaochangia ustawi wa taifa letu bila kujali itikadi za dini au misimamo ya kisiasa."

Amesema kuwa tuzo hizo zinatambua ubunifu, uongozi, mshikamano wa jamii na mchango wa wadau katika kuhakikisha elimu inakuwa jumuishi, bora na endelevu. Hili ni tukio linaloonesha kwa vitendo methali ya Mtume (S.A.W) isemayo: “tafuteni elimu hata kama ni mpaka China”; ikiashiria kuwa elimu ni chombo cha ukombozi na maendeleo ya jamii yoyote na hakuna mipaka katika kuitafuta."

Amesema Serikali kwa upande wake kupitia Dira ya Maendeleo ya 2050 imeweka malengo ya muda mrefu kuhakikisha kwamba itaendeleza ushirikiano kati ya taasisi za dini, sekta binafsi na mashirika ya kimataifa ili kuhakikisha elimu inaendelea kuwa injini ya maendeleo ya taifa.

Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa sekta binafsi, mashirika ya kidini, mashirika ya maendeleo na jamii kwa ujumla kuwekeza zaidi katika elimu. "lengo ni kuhakikisha kuwa tunawajenga vijana wetu wawe wabunifu, waadilifu na wazalishaji wa fursa za ajira badala ya watafuta ajira pekee, ongezeni uwekezaji katika elimu".

Kwa upande wake Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Dkt. Abubakar Zubeir Bin Ally, amesema kuwa tuzo hizo zimetolewa kutokana na bakwata kuthamini elimu kwa kuwa uislam ni elimu sio ujinga "Elimu ndio uhai wa uislam na ni nguzo kuu ya uslam, uislam unamchango mkubwa sana duniani katika elimu"

Kadhalika, Sheikh Dkt. Abubakar amempongeza Rais Dkt. Samia kwa usimamizi wake mzuri kwa namna anavyosimamia elimu nchini. Pamoja na hii pia tunathamini sana wadau mbalimbali wanaojitoa katika kusimamia sekta ya elimu na kutilia mkazo masuala ya elimu"

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa elimu wa Bakwata Ally Abdalah Ally amesema kuwa mpango wa tuzo hizo zilizobuniwa na Mheshimiwa Mufti zinalengo la kuinua na kuwatia moyo wadau wa elimu wanaojitoa na kujitolea ipasavyo katika mabadiliko chanya ya elimu kwa maendeleo endelevu. Katika hafla hiyo, tuzo ishirini na tatu zilitolewa.

www.ngaradc.go.tz

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • MHE COL MATHIAS KAHABI DC NGARA ATEMBELEA UJENZI WA BARABARA YA KIVUKONI RUSUMO.

    October 02, 2025
  • VIWANGO VYA UDUMAVU NA UKONDEVU VIMEPUNGUA NCHINI - MAJALIWA

    October 01, 2025
  • BONANZA LA WATUMISHI MAKAO MAKUU, WALIMU NA WANANCHI LAFANYIKA WILAYA YA NGARA

    September 27, 2025
  • CHAFANYIKA KIKAO KAZI CHA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA LISHE - 2025 WILAYANI NGARA

    September 26, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa