• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

RC CHALAMILA ATOA MAELEKEZO KWA VIONGOZI WA WILAYA, WANAFUNZI WOTE WALIOCHAGULIWA KIDATO CHA KWANZA KUWA DARASANI

Wakati ilipowekwa: January 21st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Albert Chalamila leo tarehe 21.01.2023 ametoa maelekezo kwa viongozi wa ngazi zote za Wilaya kuanzia Wakuu wa Wilaya kushirikiana na Halmashauri, Tarafa, Kata na Vijiji kufanya msako wa nyumba kwa nyumba kabla ya tarehe 31.01.2023 na kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza wawe wameripoti na kuanza masomo.


Akizungumza na waandishi wa habari, katika eneo la ofisi yake, ameeleza kuwa mzazi yoyote atakayebainika kutorosha mtoto au kufanya vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake. Pia kuanzia sasa, Wakuu wa Wilaya wapokea taarifa ya kila siku kutoka kwa Wakuu wa shule ili kuona changamoto ni nini inayopelekea wanafunzi hao wasiripoti shuleni hadi sasa.


"Kwa Mkoa wa Kagera, wanafunzi waliochagulia kujiunga na kidato cha kwanza ni wanafunzi 59,324 ambapo tulitarajia wawe wameripoti wote, hadi kufikia jana tarehe 20.01.2023 wanafunzi 35,594 sawa na asilimia 60 ya wanafunzi waliotakiwa kujiunga na kidato cha kwanza wameripoti shuleni hivyo wanafunzi 23,730 sawa na asilimia 40 bado hawajaripoti kwenye shule walizochaguliwa", ameeleza Mhe. Chalamila


Ameendelea kueleza kuwa Mkuu wa Shule yoyote atakayebainika anawakwaza wazazi kwa kuanzisha michango ambayo haipo katika utaratibu na kuweka msimamo wa kutokupokea wanafunzi kwasababu hana mchango watachukuliwa hatua za kinidhamu. Na kuwataadharisha wazazi waliowaficha watoto wao kwa maana ya kuwasaidia katika shughuli zao za kiuchumi wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya kisheria hii italeta nidhamu kwa mujibu wa Sera ya Elimu kuwa elimu hii ni ya lazima kwa mwanafunzi yoyote anayechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza.


Ameongeza kuwa kila shule iwashirikishe wazazi na kuhakikisha kuwa inatoa chakula cha mchana kama ilivyotamkwa katika waraka namba 3 wa Elimu wa Mwaka 2016 ili iwe kivutio kwa wanafunzi kubaki shule na kusoma wakiwa na utulivu hawana njaa hivyo chakula kwa wanafunzi si mchango bali ni hitaji la msingi kama ilivyo mavazi na kama ilivyo nyakati za usingizi kuhitaji kulala.


Aidha, ameeleza kuwa Mheshimiwa Rais amewekeza kwa kiasi kikubwa katika miundombinu ya madarasa pamoja na miundombinu mingine kama Maabara, matundu ya vyoo pamoja na nyumba za walimu. Pamoja na uwekezaji huo uliofanywa kwa Mkoa wa Kagera awamu ya kwanza madarasa 881 na awamu ya pili madarasa 514 ilitarajiwa kuwa kiwango cha wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwanza kiongezeke kutokana na hamasa hiyo na wanafunzi waripoti kwa wakati.


Jambo lingine alilolifanya Mheshimiwa Rais ni kuendeleza Sera ya Elimu bure kuanzia awali mpaka kidato cha sita. Kwa mantiki hiyo ilitarajiwa inapofika mwezi Januari mwaka huu wa 2023 wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza waripoti haraka shuleni kwasababu hakuna mkwamo wa madarasa na ada kama ilivyokuwa hapo awali. Hivyo kuhakikisha madarasa yaliyojengwa na Mheshimiwa Rais wanafunzi wanaripoti shuleni na wanaendelea kusoma kama ambavyo yeye amekusudia zaidi kuendeleza uwekezaji wa madarasa na ajira za walimu ili kuhakikisha elimu inayotolewa ni bora kwa kikazi cha sasa na vijavyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA TATHMINI YA UJUZI NA UZOEFU KATIKA WILAYA YA NGARA KUTOKA TEMBO NICKEL August 30, 2022
  • MREJESHO WA MPANGO NA BAJETI YA HALMASHAURI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023 KWA KAMATI YA FEDHA, UTAWALA NA MIPANGO TAREHE 12 AGOSTI, 2022 September 23, 2022
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2022 HALMASHAURI YA WILAYA YA NGARA December 04, 2022
  • RIPOTI YA ATHARI ZA KIMAZINGIRA NA KIJAMII MRADI WA MAEGESHO YA MAGARI BENAKO December 01, 2022
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • WILAYA YA NGARA YANUNUA MAGARI KUTOKANA NA FEDHA ZA MAPATO YA NDANI

    March 17, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI LAPITISHA RASIMU BAJETI YA HALMASHAURI 2023/2024 NGARA KAGERA

    March 07, 2023
  • KAMATI YA USHAURI YA WILAYA (DCC) YAPITISHA RASIMU YA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    February 22, 2023
  • MHE RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA DKT SAMIA SULUHU HASSAN ATOA PIKIPIKI KWA WATENDAJI WA KATA WILAYANI NGARA KAGERA.

    February 28, 2023
  • Tazama zote

Video

Moto Rusumo Agosti 2018
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa