• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Tatizo la Ukosefu wa Matundu ya Vyoo Lapata Muarobaini Kabanga Sekondari

Wakati ilipowekwa: January 21st, 2019

Tatizo la ukosefu wa matundu ya vyoo katika shule ya sekondari ya Kabanga Wilayani Ngara, uliokuwa unasababisha wanafunzi wa shule hiyo, kuchafua mazingira kwa kujisaidia vichakani, umepata muarobaini baada ya kufadhiliwa matundu ya vyoo 12 na tanki la maji, vilivyogharimu jumla ya shilingi milioni 47.

Ufadhili huo ulitolewa na DKT. Suzanne kutoka nchini Uingereza, ambaye alitembelea shule hiyo mwaka 2014, na kukuta upungufu wa wa matundu ya vyoo uliokuwa ukisababisha wanafunzi kuangaika kupata huduma hiyo.

Dr. Suzanne amesema amepata kiasi hicho kwa kufanya harambee kupitia shule rafiki na Kabanga Sekondari ya Les Beaucamps ya Uingereza, nchini Uingereza na kufanikiwa kupata kiasi hicho, huku akiwashukuru uongezi wa shule kwa kusimamia shughuli hiyo.

Dkt. Suzan Wilson kutoka Uingereza amesema "Maendeleo ni Afya na kwamba Maji na Afya ni Maendeleo" hivyo watumie maji na vyoo kutunza Afya zao wakijikita kusoma kwa juhudi na maarifa na kwambachangamoto nyingine zitatatuliwa na wadau mbalimbali kwa kushirikiana na serikali.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Ngara Lt. Col. Michael Mntenjele, akikagua miundombinu hiyo, baada ya kuizindua na kuikabidhi katika uongozi wa Shule, ameutaka uongozi huo kuitunza miundombinu hiyo.

Amesema kitu ambacho mzazi anaweza kumpatia mtoto wake kama urithi hapa duniani ni elimu hiyvo, akaitaka jamii ya wanangara kuwapeleka watoto wao shuleni, ili waweze kunufaika na elimu inayotolewa na serikali bila malipo iweze kuwafaidia katika maisha yao.

Akikabidhi mradi huo Januari 17, 2019; Mratibu wa Shirika la Tumanini Fund wilayani Ngara, Ndugu Alex Nyamkara, amesema ujenzi wa vyoo vitatu vyenye matundu 12, utapunguza magonjwa ya mlipuko na kuongeza mahudhurio ya wanafunzi kitaaluma.

"Mazingira ya kupata taaluma yanahitaji usalama wa kujisitiri hivyo katika vyoo vilivyojengwa kimetengwa chumba maalum kwa wanafunzi wa kike wanaopatwa na changamoto ya hedhi kila mwezi darasani" Amesema Nyamkara.

Amesema Ombi la Tanki la maji lenye thamani ya Shilingi milioni 6, na vyoo vilivyogharimu Shilingi milioni 41, lilitolewa na aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Ngara Bi. Honoratha Chitanda, baada ya ujumbe wa shule rafiki ya Les Beaucamps ya Uingereza kutembelea Kabanga mwaka 2014.

Mkuu wa shule ya sekondari Kabanga Projestus Katura, amesema shule hiyo, ilianzishwa mwaka 1990; ikiwa ya kwanza wilayani Ngara, kumilikiwa na serikali, ina wanafunzi 1,133, kati yao wasichana 630 na wavulana 503, wakifundishwa na walimu 35.

 Ameishukuru Tumaini Fund kwa ufadhili wa miundombinu hiyo, pamoja na wa kompyuta walizofadhiliwa miaka iliyopita, ingawa bado shule hiyo iana changamoto ya uhaba wa maji, vyumba vya madarasa, Bweni na kuomba kuboreshewa tanki lililopo la kuvuna maji ya mvua.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU 2024/2025 WAFANYIKA UKUMBI WA COMMUNITY CENTRE NGARA MJINI

    May 07, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE HAJAT FATMA ABUBAKARI MWASSA AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDEKEO WILAYA YA NGARA

    May 03, 2025
  • MHE HAJJAT FATMA MWASSA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO WILAYA YA NGARA

    May 02, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE HAJAT FATMA MWASSA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SHEREHE ZA WAFANYAKAZI ZAFANA KIMKOA WILAYA YA NGARA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa