• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

TFS Watakiwa Kuruhusu Halmashauri Kutumia Miti Kutengeneza Samani

Wakati ilipowekwa: December 20th, 2018

Mkuu wa mkoani wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti, ameagiza wakala wa misitu TFS kuruhusu halmashauri nane za wilaya mkoani humo, kukata miti ya kutengeneza viti na meza, kwa ajili ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2019.

Brig. Jen. Gaguti ametoa agizo hilo Desemba 20, 2018, wakati akishiriki kipindi cha Asubuhi njema kinachotangazwa na Radio Kwizera wilayani Ngara, akielezea mkakati wa kujenga vyumba 315 vya madarasa ambavyo inabidi vikamilike ndani ya miezi mitatu ijayo.

“Kutokana na changamoto ya kukosa vyumba vya madarasa, Halmashauri nimeelekeza, kutumia vyumba vya maabara, ambavyo havina vifaa vya masomo ya sayansi kwa kipindi cha miezi mitatu, kwa ajili ya kuwafundisha wanafunzi 14,046, waliofaulu na kukosa madarasa.” Alisema Brig. Jen. Gaguti.

Alisema wakala wa misitu TFS wakitoa miti, kila halmashauri itatumia mafundi wake kutengeneza samani hizo, kwa kutumia baadhi ya fedha za ruzuku zinazotolewa na serikali katika sekta ya elimu badala ya mzigo huo kuwaachia wazazi na walezi pekee.

"Mkakati wa mkoa ni kushirikisha wadau kama taasisi za kibenki na wadau wote wa elimu wenye nia njema ya kuunga juhudi za serikali kwa kutoa fedha za kujenga vyumba vipya vya madarasa,pamoja nakufanya mikutano ya harambee kwa lengo la kuondoa changamoto hiyo" Alisema Brig. Jen. Gaguti.

Pamoja na mkakati wa kutumia vyumba vya maabara, bado mkoa huo unahitaji zaidi vyumba 352 vya maabara kutosheleza mahitaji ya maabara 570, ambapo baadhi yake vilibadilishwa kutoka madarasa ya kawaida, na kuwekewa miundombinu kwa ajili masomo ya sayansi.

Baadhi ya wananchi wamemtaka mkuu huyo wa mkoa kuruhusu hata hayo majina ya wanafunzi waliofaulu, lakini hawakupata nafasi za vyumba vya madarasa kutangazwa, ili watafutiwe mahitaji ya sare na vifaa vya kujifunzia.

Mmoja wa wananchi waliopiga simu kuchangia mjadala wa kipindi cha Asubuhi njema aliyejitambulisha kwa jina la Stela Thimotheo kutokea Biharamulo; alisema wazazi wamebaki bila kujua watoto waliofaulu watakwenda shule zipi, wakati muda wa kuanza masomo Januari umekaribia.

Naye Oscar Silvester kutoka kata ya Kyebitembe wilayani Muleba, alishauri serikali ikiweka mipango na mikakati ya ujenzi wa miradi ya maendeleo, viongozi wa wilaya na wa mkoa wafike kwenye eneo husika, ili kujiridhisha na utekelezaji huku wakibaini changamoto zinazowakabili wananchi na kuzirekebisha.

Wiki iliyopita waziri wa TAMISEMI Suleiman Jaffo, alisema mikoa ya Kagera na Kigoma imefaulisha wanafunzi wengi, lakini wamekosa vyumba vya madarasa, ambapo mkoa wa Kagera unao jumla ya wanafunzi 14,046 na Kigoma wanafunzi 12,178.

Watahiniwa waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2019 mkoani wa Kagera ni watoto 39,545, ambapo wavulana ni 18, 553 na wasichana ni 20,992, huku kiwango cha ufaulu mwaka 2018 kikipanda kwa asilimia 0.02% pekee.

Mwaka 2018 mkoa wa Kagera ulikuwa na watahiniwa 47,197, waliotarajiwa kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi, kati yao wavulana walikuwa 22,124, na wasichana ni 25,073, ambapo watahiniwa 86 walikuwa wenye mahitaji maalumu; wavulana ni 50, na wasichana 36.

Mchanganuo wa wanafunzi waliofaulu, lakini hawakupata nafasi kuoka kila Halmashauri mkoani Kagera ni kama ifuatavyo; wanafunzi 2160 kutoka Biharamulo, Bukoba DC 877, Bukoba Manispaa 1276, Karagwe 3086, Kyerwa 1876, Missenyi 578, Muleba 3696 na wanafunzi 256 kutoka Ngara.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa