• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Tumieni Pikipiki Hizo Kuinua Kiwango cha Elimu; Brigedia Jenerali Gaguti

Wakati ilipowekwa: September 11th, 2018

Maafisaelimu Kata 22 katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, wametakiwa kutumia pikipiki walizopata kuinua kiwango cha elimu katika kata zao, ili wilaya ipande kielimu na kufikia nafasi ya kwanza kimkoa na hata kitaifa.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti ameyasema hayo Septemba 08, 2018 katika ofisizya Halmashauri ya Wilaya ya Ngara alipokuwa akiwakabidhi pikipiki 22 watendaji wa kata 22 katika Halmashauri hiyo.

“Ni mategemeo ya serikali kwamba mtaongeza jitihada za kusimamia elimu; mkoa wa Kagera kwa ujumla wake wilaya ya ngara ikiwemo, imekuwa na sifa nzuri ya kufanya vizuri katika masomo ya shule za msingi na za sekondari.” Alisema Brigedia Jenerali Gaguti.

Amewambia Maafisaelimu hao kuwa yeye kama mkuu wa mkoa anapowakabidhi pikipiki hizo anatarajio kuona ubora wa elimu katika mkoa wa Kagera unaongezeka; na kuogeza kwamba kuanzia mwaka 2019 mkoa utachukua nafasi ya kwanza katika kufaulu mitihani ya darasa la saba kitaifa.

Kwa mkuu wa mkoa huyo kikubwa ni walimu kusimamia na kufuata taratibu, kanuni na maadili ya kazi ya ualimu, likiwemo suala la utoaji adhabu kwa wanafunzi, na kudai kwamba asingependa kuona tatizo lililotokea katika Manispaa ya Bukoba litokee tena katika Mkoa wa Kagera.

Amesema walimu wamepewa dhamana kubwa ya kusimamia elimiu na kuhakikisha kwamba mifumo ya elimu, iliyowekwa na serikali inasimamiwa na kuzingatiwa vizuri; huku akiwataka maafisaelimu hao kutumia vyombo hivyo kuthibiti utoro wa wananfunzi katika shule zote za msingi Wilayani.

“Tumepewa vifaa hivi tuvitunze vifanye kazi leo, vifanye kazi kesho na siku zote zijazo, ili elimu iendelee kuwa bora siyo katika mkoa wa Kagera tu, bali katika taifa zima.” Alisisitiza Mkuu huyo wa Mkoa wa Kagera.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama amesema kwamba pikipki hizo si za kufanya kazi binafsi, bali zimetolewa na serikali kwa ajili ya kwenda kufanya ufuatiliaji wa shughuli za maendeleo ya elimu katika kata zao.

Mkuu wa Kagera amekabidhi pikipiki 22 kwa Maafisaelimu Kata 22 Septemba 08, 2018 wakati alipokuwa katika ziara ya kujitambulisha kwa watendaji wa mkoa wa Kagera, ili aweze kujua matatizo ya wananchi na kuyatafutia ufumbuzi.

Katika Ziara yake Wilayani Ngara alipata nafasi ya kutembelea mradi wa afya katika kata ya Mabawe, ambapo aliongea na wananchi, kutembelea kiwanda cha kukoboa kahawa cha Ngara Coffee, kuongea na watumishi wa Halmashauri, wafanyabiashara na kuhitimisha ziara yake kwa kukabidhi pikipiki kwa maafisaelimu 22.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa