• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Ufaulu wa Wanafunzi wa Sekondari Wilayani Ngara Wapanda kwa 79%

Wakati ilipowekwa: March 7th, 2018

“Kwa kuzingatia matokeo ya mitihani ya taifa ya wanafunzi wa kidato cha nne kwa miaka mitatatu mfululizo, hali ya kitaaluma katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara inaridhisha.” Alisema Kaimu Afisaelimu idara ya sekondari ndugu Marton James akiwa ofisini kwake.

Afisaelimu James amesema ufaulu umeongezeka kwani kuanzia mwaka 2015 hadi 2017, ufaulu wa wanafunzi umeogezeka na kufikia wastani wa 79%, ikilinganishwa na ufaulu wa mwaka 2015, ambapo wanafunzi wa kidato cha nne walifaulu kwa wastani wa 67% pekee.

“Kutokana na matokeo hayo Halmashauri yetu imefanikiwa kushika nafasi zifuatazo kimkoa mwaka 2015 ilikuwa ya nne (04), mwaka 2016 ilikuwa ya nne (04) ambapo mwaka 2017 ilikuwa ya tatu (03) kati ya Halmashauri nane (08) za mkoa wa Kagera.” Alisema afisaelimu huyo.

Aidha, amesema mbali na kufanya vizuri katika mithani ya kitaifa; kila Tarafa ina shule ya kidato cha tano na cha sita na kila kata inamiliki shule ya sekondari, isipokuwa kata moja ya Nyamagoma aliyoitaja kuwa ni mpya.

Akijibu swali kwa nini mafanikio hayo, alisema yanafuatia juhudi mbalimbali alizozitaja kuwa ni ufuatiliaji na usimamizi wa ufundishaji na ujifunzaji katika shule za sekondari.

Hata hivyo amesema kuwa utoro, maadalizi hafifu ya ufundishaji, umbali mrefu wa makazi ya wanafunzi na walimu, ni baadhi ya changamoto zinazorudisha nyuma juhudi zao.

Afisaelimu huyo ameongeza kuwa wanakabiliana na changamoto hizo kwa kutoa hamasa kwa wazazi na wanafunzi ili watambue umuhimu wa elimu, wakuu wa shule wameelekezwa kusimamia mahudhurio ya wanafunzi ili kudhibiti utoro wa rejareja, pamoja na kuwatuza wanafunzi wanaofanya vizuri katika mitihani yao.

Halmashauri ya Wilaya ya Ngara kupitia idara ya elimu sekondari inasimamia taaluma katika shule za sekondari 29, amabapo shule 23 zinamilikiwa na serikali na shule sita zinamilikiwa na sekta binafsi. Pia inamiliki shule moja pekee yenye kidato cha tano na cha sita.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU 2024/2025 WAFANYIKA UKUMBI WA COMMUNITY CENTRE NGARA MJINI

    May 07, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE HAJAT FATMA ABUBAKARI MWASSA AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDEKEO WILAYA YA NGARA

    May 03, 2025
  • MHE HAJJAT FATMA MWASSA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO WILAYA YA NGARA

    May 02, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE HAJAT FATMA MWASSA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SHEREHE ZA WAFANYAKAZI ZAFANA KIMKOA WILAYA YA NGARA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa