• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Ukosefu wa Maadili ya Kazi Vinapelekea Ukiukwaji wa Haki za Binadamu; Fr. Afulo Jr

Wakati ilipowekwa: January 24th, 2019

Ukosefu wa maadili mema kiutendaji, misingi ya utawala bora pamoja na ikiukaji wa sheria kwa baadhi ya viongozi katika mataifa mbalimbali Afrika, ni baadhi ya vikwazo vinavyohatarisha haki za binadamu na kukosekana kwa amani ya kudumu barani humu.

Mkuu wa shirika la Mapadre wa Yesu (Jesuit Fathers) Afrika mashariki, Padre Joseph Oduor Afulo, amebainisha hayo Januari 22, 2018, baada ya kutembelea wilaya ya Ngara mkoani Kagera, kuwahamasisha mapadre waliojiunga na shirika hilo, ili baadae waweze kudumisha amani na utulivu watakapoanza kazi za kiroho.

Shirika la mapadre hao ukanda wa Afrika Mashariki unajumuisha nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Ethiopia, Sudani kusini na kaskazini, ambapo kazi yao kubwa ni husimamia miradi ya elimu, Afya, huduma kwa wakimbizi (Jesuit Refugees Service), amani na maridhiano na kuhamasisha haki za binadamu barani Afrika.

Padre Afulo amesema bara la Afrika limepoteza amani na utulivu kutokana na viongozi wenye dhamana kutofuata misingi ya utawala bora, kukuza demokrasia lakini pia baadhi yao hawatumii kanuni na sheria kulinda maslahi ya mataifa wanayoyaongoza baada ya kupatiwa dhamana na wananchi au mamalaka zinazohusika.

"Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo, wanaokiuka haki za binadamu wanakosa malezi kifamilia, kutokuwa na adabu na utii na kukiuka misingi ya kiroho, ndiyo hao hao katika makanisa na misikiti licha ya kuonekana watu wema mchana, lakini usiku wanafanya kinyume" Amesema Afulo

Alisema mataifa mengi yamekosa mwelekeo wa amani na utulivu yemejaa mateso, kuwepo changamoto ya vurugu za kisiasa, kiuchumi na kijamii lakini pia utendaji wa viongozi wa kisiasa umekuwa wa kujichukulia maamuzi badala ya kufuata waliyotumwa na waliowachagua.

Ameshauri viongozi duniani hasa wenye mamlaka wawe wakweli katika kutamka na kutenda, ili  kudumisha amani badala ya kusababisha machafuko, vita na dhuluma na kila mmoja aguswe na tatizo la mwingine kwa kuanzia ngazi ya familia ili kuwepo usalama kila taifa.

Mesikitishwa na mifumo ya elimu inayotolewa hivi sasa kwa wanafunzi kwamba haihamasishi viongozi mbalimbali duniani kuwajenga wananchi kujitegemea, matokeo yake wanasababisha matabaka, kwani watoto wa viongozi husomea katika shule zenye gharama kubwa; huku wakiwa tegemezi kiakili.

Kabla ya uhuru wanafunzi walijifunza elimu ya kujitegemea, kwa sasa wanalundikiwa masomo mengi, wakijifunza kujibu mitihani kuanzia elimu ya awali hadi chuo kikuu, na kila anayepata nafasi, anakuwa fisadi kwa kila mbinu, ili kujinufaisha.

"Inafaa wazazi kuwalea watoto kwa nidhamu maana aja ya mja hunena; lakini kutolewe elimu ya kujitegemea, kuepuka kupata viongozi na watendaji mafisadi, wala rushwa na wenye kukiuka haki za wengine" Aliongeza.

Akiwa wilayani Ngara aliwapongeza wandishi wa habari wa Radio Kwizera, kwa utendaji kazi wao katika kuhabarisha jamii na kuhimiza utawala bora, upatikanaji wa haki za binadamu na kwamba lengo la ziara yake nchini Tanzania ni kujua hali ya majesuit kwa huduma wanazofanya hapa nchini.

Awali akiwa na wenyeji wake wilayani Ngara Padri Fredrick Meela, alisema katika kusimamia majukumu na utendaji wa shirika hilo, kwa wilaya ya Ngara na wilaya zinazounda mkoa wa Kigoma, wananchi wanapata huduma za kuwajenga kiroho na kuwapa matumaini.

Alisema upashanaji wa habari hupitia njia ya Radio Kwizera kwa kuweka wanahabari maeneo mbalimbali, zikiwemom kambi za wakimbizi mkoani Kigoma; lakini hata maeneo mengine kwa baadhi ya mikoa ya kanda ya ziwa Viktoria.

Amesema pia mapadre hao wanasimamia elimu maeneo mbalimbali nchini kama vile Loyola iliyoko Mabibo jijini Dar es Salaam, St Peter Claver ya mkoani Dodoma zikiwemo shule za msingi lakini pia shule hizo hutoa huduma za afya kwa ajili ya wanafunzi na walimu.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa