• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

WAFANYABIASHARA WA MAFUTA ZINGATIENI MAISHA YA WANANCHI - DKT. BITEKO

Wakati ilipowekwa: February 7th, 2024

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Chama cha Waagizaji na Wasambazaji wa Mafuta nchini (TAOMAC) ambapo amewataka wafanyabiashara hao pamoja na faida wanayoipata wazingatie maslahi wananchi wa hali ya chini.

Ameyasema hayo tarehe 06 Februari, 2024 jijini Dodoma katika kikao ambacho kilijadili masuala mbalimbali ikiwemo changamoto mbalimbali ambazo wanafanyabiashara hao wanazikabili.

Amesema Serikali siku zote iko tayari kutoa ushirikiano kwa wafanyabiashara na kuwekea mazingira wezeshi ya biashara zao ili waweze kuwajibika kwa mujibu wa sheria kanuni na taratibu za usimamizi katika sekta husika.

“Tunapofanya biashara hii ya mafuta lazima tuangalie mtanzania maskini ambaye anategemea sekta hii kujikwamua kimaisha, isifike mahala kila mwisho wa mwezi watu wote wanashika vichwa wakihofia kupanda kwa bei ya mafuta… Serikali inafanya kila jitihada kupunguza makali ya bei ya mafuta hivyo nanyi mlizingatie suala hili.”amesema Dkt. Biteko.

Dkt. Biteko ameishukuru TAOMAC kwa ushirikiano wao kwa Serikali katika kuhakikisha kuwa nchi inakuwa na mafuta ya kutosha na kueleza kuwa Serikali inatambua na kuthamini mchango wao katika ukuaji wa Uchumi wa nchi.

Amesema uhusinao uliopo kati ya Serikali na TAOMAC unahitaji kuwa endelevu na pale zinapotokea changamoto zitafutwe njia za kukabiliana nazo kwa mstakabali wa Taifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa TAOMAC, Kalpesh Mehta ameishukuru Serikali kwa mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara wa mafuta na utayari wa Serikali kushughulikia changamoto kadhaa zinazojitokeza katika sekta hiyo.

Akizungumzia mazingira hayo, Mkurugenzi Mtendaji, Raphael Mgaya amesema ushirikiano wa TAOMAC kwa serikali hauepukiki ili kuhakikisha nchi inapata mafuta ya kutosha hivyo wapo tayari kushirikiana na Serikali.

Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Watendaji kutoka  Taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Benki Kuu  ya Tanzania (BoT) Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), Shirika la Uwakala wa Meli (TASAC), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba.

ngaradc.go.tz

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa