• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Wajumbe Waridhishwa na Upanuzi wa Barabara za Mitaa Ngara Mjini

Wakati ilipowekwa: November 21st, 2018

Kamati ya fedha, Mipango na Uongozi imeridhika na zoezi la kupasua na kupanua barabara za vitongoji vya Mji wa Ngara, linalofanywa na Tanzania Rural and Urban Roads Agency (TARURA), kwa kushirikiana na Halmashauri kwamba linarahisisha upatikanaji wa huduma za jamii.

Haya ameyasema Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Erick Nkilamachumu, wakati akihitimisha ziara ya siku mbili iliyofanyika Novemba 19, 2018 ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri hiyo, ,.

“Kwenye suala la barabara changamoto hazikwepeki; kwa sababu tunapopanua barabara tunalazimika kukata migomba, miti na saa nyingine kubomoa baadhi ya nyumba za wananchi, kwa hiyo, lazima lawama ziwepo, lakini lazima tukabiliane nazo.” alisema Ndugu Nkilamachumu.

Amewataka wataalamu kwa kushikiana na Mkurugrnzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama, wawasiliane na TARURA, waone jinsi watakavyoweka changarawe na kalavati, ili barabara hizo zipitike wakati wa mvua na kiangazi.

Aidha, amesema wananchi lazima wahamasishwe na kuelimishwa umuhimu wa zoezi hili, kusudi waweze kuhiari kutoa maeneo yao, yatumike katika kupanua na kutengeneza barabara za mji; kwani kufanya hivyo kutarahisisha usambazaji wa huduma za jamii kwa wananchi.

Naye, Kaimu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Bi. Georgia Munyonyera, ameishukuru Halmashauri na TARURA, kwa kazi hiyo kubwa na nzuri ya kupasua barabara za mitaa katika maeneo mbalimbali, huku akiomba zoezi hilo liendelee katika vitongoji vingine.

Barabara hizo ni msaada mkubwa, kwa sababu zitarahisisha maisha ya wananchi na kuongeza thamani ya viwanja vyao baada ya kuvipima, huku akitoa ushauri wa jinsi ya kukabiliana na changamoto zinazojitokeza, hasa kuhusiana na mashamba ya watu ambako barabara hizo zinapita.

“Nitoe wito kwa wataalamu wa maedeleo ya jamii na ofisi ya mamlaka ya mji mdogo, wawashauri na kuwahamasisha wananchi juu ya umuhimu wa barabra hizo kwao, ili wawaruhusu na kama kuna tatizo basi tulitatue kabla.” Alisema Bi Munyonyera.

Ziara ya siku mbili ya wajumbe wa kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi, walitembelea miradi Maendeleo; ukamilishaji wa maabara katika shule za sekondari za Murugwanza na Kanazi, Kituo cha Afya cha Mabawe, na vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi ya Rulenge vilivyojengwa kwa msaada wa Jambo Bukoba na Halmsahauri kwa gharama ya shilingi milioni 23.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa