• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Wanafunzi 25 Waacha Shule Kwa Sababu ya Kupata Mimba

Wakati ilipowekwa: December 13th, 2018

Wanafunzi 25 wa shule za sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, wameacha shule kwa sababu ya kupata ujauzito, na hakuna mhusika aliyekamatwa kwa kusababisha tatizo hili, ingawa kesi hizo zimeripotiwa kituo cha polisi.

Kaimu Afisaelimu Idara ya Sekondari wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara Ndugu James Marton, amekiambia kikao cha watendaji, wakuu wa shule za sekondari na msingi, na maafisaelimu kata wakati wa kikao kazi cha maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wa kidato cha I na wa darasa la I mwaka 2019.

“Kwa mwaka jana na mwaka huu takwimi tulizonazo jumla ya wanafunzi 25, wameacha shule, kwa sababu ya mimba; nawaomba watendaji wote, tulifanyie kazi kwa sababu hamna kesi yoyote, ambayo imeisha hukumiwa kati ya hizi.” Alisema Ndugu Marton.

Afisa huyo alisema tatizo hili ni kubwa, kwani idadi ya wanafunzi waliopotea kwa sababu ya mimba ni nusu ya darasa moja, huku akisema kwamba anatoa taarifa hiyo, ili watendaji pamoja na wakuu wa shule wajue hali halisi ilivyo.

Amezitaja shule zilizoathirika kwa tatizo la ujauzito zikiongozwa na kata ya kibimba, kuwa ni shule ya sekondari Rusumo ‘B’ wanafunzi 02, Shunga wanafunzi 03, Kanazi mwanafunzi 01, Mabawe mwanafunzi 02, Kibimba wanafunzi 04, na shule ya sekondari Murusangamba wanafunzi 03.

Shule nyingine ni Ndomba wanafunzi 02, Bukiriro wanafunzi 03, Rusumo wanafunzi 02, Ngara mwanafunzi 01, Muganza mwanafunzi 01, pamoja na Kirushya mwanafunzi 01 na kuongeza kwamba baadhi ya kesi hizi ziko polisi, wakati nyingine hazijulikani zilipo.

Baada ya taarifa hiyo, Afisa Tawala wa Wilaya ya Ngara Ndugu Vedastus Tibaijuka alisema suala la mimba katika shule za sekondari na msingi ni tatizo kubwa, kwani kuna wastani wa wanafunzi 10 kwa mwezi walipata ujauzito.

“Suala la mimba wastani wake kwa wilaya yetu ni mbaya, ukilinganisha na wilaya nyingine, tulipokaa kamati ya ulinzi na uslama ripoti kwa mwezi kwa wastani katika shule ya msingi na sekondari watoto wapatao 10, walipata ujauzito kwa mwezi; hili linatukwaza.”

Hili tatizo ni kubwa sana; wilaya nyingine watu wengependa kuwaheshimu wanafunzi, lakini kwa ngara wangependa kuoa, au kutembea na wanafunzi, kinachosikitisha zaidi wanaofanya vitendo hivyo ni watu wazima.

Amesema kesi zinaripotiwa polisi lakini zinapotea kwa sababu wazazi wanaficha ukweli na hawako tayari kutoa ushahidi; “kesi za mimba zikianza hivyohivyo, nyingi zinaishia kwenye vijiji na kata mtoto anapotea mzazi hayuko tayari kutoa ushirikiano.” Alisema Ndugu Tibaijuka.

Akitoa mfano, alikiambia kikao hicho kwamba anakumbuka wakati anasoma, mwalimu na Matroni walikuwa na uwezo wa kubaini watoto fulani Fulani, wenye wenye tabia mbaya wanawaonya kabla na matokeo yake yalikuwa mazuri sana.

Hata hivyo wasimamizi hao wa elimu, walisema tatizo la mimba linasababishwa na watoto kutembea umbali mrefu, huku wakidai kwamba wanafunzi hao wanapopanga vyumba, wazazi hawawahudumuii wala kuwatembelea, ili kujua mahitaji yao ya msingi.

Kwa maoni yao kujenga mabweni shuleni hasa kwa ajili ya watoto wa kike linaweza kuwa suluhisho la kudumu, kwani watoto hao watakuwa chini ya uangalizi wa walimu; huku wakiongeza kwamba pia itawasaidia kujifunza kwa umakini zaidi.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU 2024/2025 WAFANYIKA UKUMBI WA COMMUNITY CENTRE NGARA MJINI

    May 07, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE HAJAT FATMA ABUBAKARI MWASSA AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDEKEO WILAYA YA NGARA

    May 03, 2025
  • MHE HAJJAT FATMA MWASSA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO WILAYA YA NGARA

    May 02, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE HAJAT FATMA MWASSA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SHEREHE ZA WAFANYAKAZI ZAFANA KIMKOA WILAYA YA NGARA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa