• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Wanafunzi Waisifu Serikali kwa Kuwajengea Madarasa na Mabweni

Wakati ilipowekwa: May 28th, 2018

Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Murugwanza katika Halmashauri ya wilaya ya Ngara wameishukuru serikali kwa kuwajengea madarasa manne, mabweni mawili pamoja na kukarabati maabara za biolojia, kemia na fizikia.

Shukurani hizo walizitoa kwa Mkurugenzi Mtandaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama, alipotembelea shule hiyo wakati alipofanya ziara ya kutembelea miradi ya afya na elimu, ili kujiridhisha na maendeleo ya miradi hiyo Mei 24, 2018.

Wanafunzi hao wamesema mabweni yamewasaidia wanafunzi waliokuwa wakiishi mbali na shule, kuwahi vipindi darasani, kuwa na utulivu wa mawazo, kujisomea kwa bidi pamoja na kupata nafasi ya kujadili masomo na wanafunzi wenzao.

“Sisi wanafunzi wa kike tulikuwa tunapata shida sana, mbali na kutembea umbali mrefu kuja shuleni, njiani tulikuwa tunakutana na vishawishi vingi, lakini sasa tunatarajia kufanya vizuri katika mitihani yetu baada yak upata nafasi ya kulala shuleni.” Mwanafunzi mmoja wa kike alimwambia Mkurugenzi Mtendaji.

Aidha, walisema kuwa bado tatizo la upungufu wa mabweni lipo, kwani wanafunzi wengi bado wanatembea umbali mrefu kuja shuleni, kwa sababu hiyo wengi uchelewa kuhudhuria vipindi vingi vya kwanza.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri wa Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama, amesema mradi wa ujenzi wa mabweni mawili (02) yenye uwezo wa wanafunzi 80 kila moja, madarasa manne (04), na ukarabati wa maabara vimegharimu shilingi 292,000,000/=.

Amewaambia wanafunzi hao kuwa serikali inalengo la kujenga mabweni ya wanafunzi kwa kila shule, lakini itafanya hivyo kwa awamu, hivyo aliwataka wanafunzi hao kuwa wavumilivu, wakati serikali inajipanga kukamilisha mabweni katika shule zao.

Mkurugenzi Mtendaji alikuwa na ziara ya kukagua miradi ya maendeleo, inayojengwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Mei 22-25, 2018 na kulidhishwa na maendeleo ya miradi hiyo, kwani yote ipo katika hatua za usafi.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU 2024/2025 WAFANYIKA UKUMBI WA COMMUNITY CENTRE NGARA MJINI

    May 07, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE HAJAT FATMA ABUBAKARI MWASSA AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDEKEO WILAYA YA NGARA

    May 03, 2025
  • MHE HAJJAT FATMA MWASSA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO WILAYA YA NGARA

    May 02, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE HAJAT FATMA MWASSA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SHEREHE ZA WAFANYAKAZI ZAFANA KIMKOA WILAYA YA NGARA

    May 01, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa