• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Wasimamizi wa Elimu Wilayani Ngara Watakiwa Kuthibiti Utoro Mashuleni

Wakati ilipowekwa: December 12th, 2018

Wakuu wa shule za sekondari, Maafisaelimu Kata, Watendaji wa Kata na Vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, wametakiwa kuchukua hatua za kudhibiti utoro shuleni, kulikopelekea wanafunzi wapatao 673 kutoroka katika kipindi cha 2017 na 2018.

Hayo ni kwa mujibu wa Kaimu Afisaelimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Marton James, wakati wa kikao kazi cha maadalizi ya kuwapokea wanafunzi wa kidoto cha kwanza na wa darasa la kwanza 2019, kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri Desemba 05, 2018.

“Kuna utoro uliokithiri katika shule zetu za sekondari watoto wengi wanapotea, na mnajua serikali inatoa gharama kubwa, kwa ajili ya kuwasomesha wanafunzi hawa; katika mwaka 2017 na 2018 tumepoteza jumla ya wanafunzi 637.” Alisema Ndugu Marton.

Amefafanua kwamba kati ya wanafunzi hao; wavulana waliotoroka ni 340, ambapo wasichana wapatao 297 wametokomea, huku akizitaja shule zinazoongoza kwa utoro kuwa ni shule ya sekondari Bukiriro iliyopoteza wanafunzi 112.

Shule nyingine zinazoongoza kwa utoro ni shunga na Nyakisasa sekondari, lakini hakutaja idadi ya wanafunzi watoro; huku akiwataja wanafunzi wa shule ya Kibogora kuwa ni 58, Rusumo imepoteza wanafunzi 52, Ngara sekondari wanafunzi 57, na Muyenzi imepoteza wanafunzi wapatao 33.

Amewapongeza wakuu wa shule za sekondari za Ntobeye, Nyabisindu, na Lukole kwa kudhibiti utoro, kwa madai kwamba vyanzo vyao vya taarifa vinaoonyesha shule hizo ndizo pekee, ambazo wanafunzi hawatoroki shuleni.

Aidha, amefafanua kwamba wanafunzi aliowataja kuwa watoro, wameacha kusoma kwa muda wa siku tisini, yaani miezi mitatu mfululizo bila kuhudhuria shuleni; “utoro ninaozungumzia mwanafunzi, akishakaa nyumbani zaidi ya siku 90, huyo siyo mwanafunzi tena.” Alisema Ndugu Marton.

Mkuu wa shule ya sekondari ya Kibogora Mwalimu Aquiline Gwimo, akichangia hoja alisema moja ya sababu za utoro, wanafunzi kutembea mwendo mrefu, kutoka shuleni hadi nyumbani, kwani umbali huo unawachosha wanafunzi, wengine wanakata tamaa na kuamua kuacha shule.

Ameshauri kuwepo mpango wa kujenga mabweni, kwani hayo yatawasaidia wanafunzi kusoma kwa utulivu, huku walimu wakiwa na nafasi nzuri ya kuwadhibiti wakati wote wanapokuwa shuleni.

Aidha, wazazi wametuhumiwa kwa kuchangia katika tatizo hili, kwa madai kwamba hawawafuatilii watoto wanaporejea nyumbani wakati ambao si wa likizo, ili wajilidhishe ni kwa nini mtoto hayupo shuleni.

Naye Afisa Tawala wa Wilaya ya Ngara Ndugu Vedastus Tibaijuka, amekiri kuwepo kwa tatizo hilo, na kuwataka maafisaelimu kata na wakuu wa shule za sekondari, kuliona tatizo hili na kulichukulia kwa uzito unaostahili na kulidhibiti.

“Mambo haya yanasikitisha sana, jamii yetu ya ngara, wazazi wanapenda watoto wafanyekazi za ndani, mtoto anakuwa darasa la tano au la sita, mzazi ameisha muadalia mazingira ya kwenda kufanyakazi ndani Kahama au sehemu nyingine.” Alisema Afisa Tawala Tibaijuka.

Ameitaka jamii ibadilika na ione umuhimu wa elimu kwa watoto wao, huku akisistiza kwamba Ngara haiwezi kuendelea kuwa duka la watoto wa kufanyakazi za ndani, bali iwe kitovu cha watoto wasomi.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa