• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Wekeni Mikakati ya Kupunguza Utoro Shuleni

Wakati ilipowekwa: July 17th, 2018

Wakuu wa shule za sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara wametakiwa kuweka mikakati ya kupunguza utoro wa wanafunzi ili kuinua kiwango cha kufaulu wilayani humo.

Haya yamesemwa na Afisa Elimu Takwimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Zacharia Mkumbo, wakati wa kikao kazi cha walimu wakuu wa shule za sekondari, kilichoandaliwa na Idara ya Elimu Sekondari kilichofanyika shule ya sekondari Ngara Julai 12, 2018.

“Kama wakuu wa shule tujiwekee mkakati wa kukomesha utoro ili takwimu za kufikia machi mwaka kesho zishuke, kwa sababu hadi sasa kila mmoja wetu anajua yuko wapi na anatakiwa kufanya nini ili kutimiza azma hiyo.” Alisema Ndugu Mkumbo.

Shule zinazoongoza kwa utoro ni Bukiriro yenye watoro 112, Shunga wanafunzi 80, Kibogora wanafunzi 58, Muganza wanafunzi 57, shule nyingine ni Rusumo yenye wanafunzi 52.

Amewataka wakuu hao wa shule kuwahimiza walimu wa madarasa, kuripoti na kuwafuatilia wanafunzi watoro na kuwarejesha shuleni, ili wasipoteze na kukosa haki yao ya msingi ambayo ni elimu.

Ndugu Mkumbo amesema walimu wa madarasa ni zaidi ya wazazi kwani wana muda mrefu wa kukaa na wanafunzi; hivyo wanawajibika kuhakikisha wanafunzi wote wanahudhuria shuleni hadi watakapohitimu masomo yao.

Naye Kaimu afisaelimu sekondari Ndugu Marton James amewakumbusha walimu wakuu wakomeshe tabia ya baadhi ya walimu shuleni kwao, wenye tabia ya kuwatukana watoto kwa madai kwamba tabia hiyo inawakatisha tamaa wanafunzi.

Amesema kwamba walimu wenye tabia hiyo wanaweza kuwa ndio chanzo cha uturo uliokithiri wa wanafunzi kwani hadi Machi 2018, wanafunzi wapatao 674 wameacha shuleni na kutokomea kusikojulikana.

Afisaelimu taaluma amewasisitiza wakuu hao kuwakumbusha walimu wao kujaza nyaraka muhimu za kufundishia zikiwemo adalio la somo, kujaza shajala za masomo pamoja na kuita majina kila siku ili kubaini wasiohudhuria shule.

Walimu wa kuu wameishukuru ofisi ya elimu sekondari kwa kuandaa kikao hicho ambacho kwao kimekuwa cha manufaa kwani wameweza kushirikishana kimawazo; huku wakikemea pale pasiponyooka.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa