• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

KAGERA YASIFIWA KWA KULINDA AMANI: RC FATUMA MWASSA AWASHUKURU WANANCHI, IJUKA OMUKA 2025 YAZINDULIWA RASMI

Wakati ilipowekwa: December 18th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Hajjat Fatuma Mwassa, amewapongeza na kuwashukuru wananchi wa mkoa huo kwa kuilinda heshima ya Kagera na Taifa kwa ujumla, hususan katika kipindi cha Uchaguzi na baada ya uchaguzi, kwa kudumisha amani na kuonesha uzalendo wa hali ya juu.

Akizungumza Desemba 18, 2025, wakati wa ufunguzi wa Tamasha la Ijuka Omuka 2025 sambamba na Dua na Sala ya Kuliombea Taifa, Mkuu wa Mkoa alisema Kagera imeendelea kuwa mfano wa kuigwa kitaifa katika kulinda amani.

“Niwashukuru sana wana Kagera; mlionesha uzalendo mkubwa katika kipindi chote tulichopita kama Taifa. Hamkushiriki kwa namna yoyote katika vitendo vya uvunjifu wa amani,” alisema.

RC Mwassa aliwasihi wananchi kuendelea kuwa mabalozi wa amani kwa Watanzania wengine, akisisitiza kuwa historia ya Kagera imejaa mafunzo makubwa kutokana na nyakati ngumu ilizowahi kupitia.

 “Tumepitia Vita ya Kagera ya mwaka 1978, maambukizi ya UKIMWI, kuzama kwa Meli ya MV Bukoba, tetemeko la ardhi na ajali ya ndege. Haya ni majonzi makubwa, hatutamani yajirudie tena,” alisisitiza.

Aidha, alisema Tamasha la Ijuka Omuka 2025 linalenga kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji mkoani Kagera, kuchochea maendeleo ya kiuchumi, kuimarisha mshikamano kupitia Bonanza la Michezo, pamoja na kuenzi utamaduni wa Kagera ikiwemo vyakula vya asili.

Kwa upande wake, akitoa salamu kwa niaba ya viongozi wa dini, Askofu Ayubu Silivester, Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste Mkoa wa Kagera (CPCT), aliwahimiza wasomi, wataalamu na wawekezaji kuikumbuka Kagera kama nyumbani na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya mkoa huo.

Tamasha la Ijuka Omuka 2025 limeanza rasmi Desemba 18, 2025, mjini Bukoba, na linatarajiwa kuhitimishwa Jumapili, Desemba 21, 2025, likibeba kaulimbiu isemayo

“IJUKA OMUKA  WEKEZA KAGERA, IRUDISHE KATIKA UBORA WAKE (Make Kagera Great Again)"

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DKT. MWIGULU ANAZUNGUMZA NA MACHINGA, MADEREVA PIKIPIKI NA BAJAJI

    January 08, 2026
  • SALAMU ZA MWAKA MPYA KUTOKA KWA DED NGARA

    January 01, 2026
  • SALAMU KUELEKEA MWAKA MPYA 2026

    January 01, 2026
  • COL KAHABI DC NGARA AKAGUA MPAKA WA TANZANIA NA RWANDA UNAOTENGANISHWA NA MTO KAGERA

    December 24, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa