• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI KIMKOA YAFANYIKA WILAYANI NGARA

Wakati ilipowekwa: December 1st, 2022

Mkoa wa Kagera, leo tarehe 01 Desemba umeungana na Nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kuadhimisha siku ya UKIMWI Duniani, ki Mkoa Wilayani Ngara katika viwanja vya Posta Ya zamani  Ngara Mjini ambapo Mgeni rasmi wa maadhimisho hayo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Albert Chalamila.


Katika maadhimisho hayo, Mhe. Chalamila amekagua mabanda mbalimbali ya wadau na mashirika yanayojishughulisha na huduma za afya hususani yanayopambana dhidi ya maambukizi ya UKIMWI. Ambayo ni MDH, PACT, TADEP, HUMULIZA na AMREF.


Katika hotuba yake kwa wananchi, Mhe. Chalamila ameeleza kuwa kundi linaloongoza kuwa na maambukizi mapya ni kundi la vijana wenye umri wa kati ya miaka15 hadi 24 hali ambayo ni tishio kwa nguvu kazi na Israël wa Taifa letu.


“Katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani, Mkoa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali waliopo tumedhamiria kwa pamoja kupambana na tatizo hili hadi kufanikisha kutokomeza kabisa katika Mkoa wetu. Kwa upimaji uliofanyika kwa kipindi cha mwaka 2022 kuanzia mwezi Januari-Novemba 15,2022, kiwango cha maambukizi mapya kimepungua hadi kufikia asilimia 2,” ameeleza RC Chalamila.


Aidha, katika kufikia malengo ya mkakati wa 95, 95, 95 (tisini na tano tatu) mpaka kufikia mwezi Septemba, 2022 asilimia 97.85 ya lengo la asilimia 95 ya watu wanaokadiriwa kuishi na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI walikuwa wamefikiwa na asilimia 97.3 ya walioanza kutumia dawa za kufubaza Virusi vya UKIMWI walikuwa na virusi vilivyofubaa.


Sambamba na hayo ameeleza juu ya changamoto mbalimbali katika kufikia asilimia 95 ya kwanza ya kimamkati, kwa upande wa wanaume kutokujitokeza katika upimaji ukilinganisha na wanawake, maeneo mengi kutofikika kwa huduma zote za afya hasa upimaji, kutokutaja kwa mshirika wa ngono ili aweze kupimwa na unyanyapaa. Serikali imeendelea kupambana na changamoto hizo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.


Amewaomba wananchi wote wa Mkoa wa Kagera kuwa na tabia ya kupima afya kila mara na kusisitiza Kamati zote za UKIMWI katika ngazi zote Zifanye kazi, takwimu ziandaliwe na kuwekwa wazi kwa kila eneo na elimu ya kujikinga na maambukizi iendelee kutolewa zaidi kupitia vyombo vya habari vilivyopo Mkoani Kagera.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa