• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Ndugu Bahama; Pikipiki ya Serikali Aipotei Wala Kuibwa

Wakati ilipowekwa: September 8th, 2018

“Natamuka rasmi kwamba pikipiki ya serikali aipotei wala kuibwa; itakayopotea au kuibwa ni pikipiki binafsi ya Afisaelimu Kata.” Alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama.

Ndugu Bahama, ameyasema hayo wakati akipokea pikipiki 22, kofia ngumu 22 na ‘groves’ 22, vilivyopokea toka Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknojia Septemba 07, 2018 kwa lengo la kuwasaidia Mafisaelimu Kata kusimamia ubora wa elimu katika Kata zao.

Ndugu Bahama amesema serikali imetoa pikipiki hizi kwa Maafisaelim Kata, ili waweze kusimamia ubora wa elimu kupitia mpango wa kukuza stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu KKK.

“Kama zilivyo Halmashauri nyingine hapa nchini ambazo zilikuwa na tatizo la watoto wa shule za msigni kushindwa kusoma, kuandika na kuhesabu, Halmashauri ya Ngara nayo bado inachangamoto hiyo, lakini naamini pikipiki hizi zitakuwa msaada mkubwa katika kutokomeza tatizo hili.” Alisema Mkurugenzi huyo Mtendaji Ndugu Bahama.

Alisema kuwa wanapokea pikipiki hizo kama sehemu ya serikali katika kutekeleza sera ya elimu ya mwaka 2014, inayomtaka mtoto wa kitanzania amalizapo elimu ya msigi awe na maarifa, mahiri, na uwezo wa kuleta maendeleo yake binafsi na ya taifa.

Ndugu Bahama anaishuskuru serikali kwa kuamua kutoa pikipiki hizo alizosema, kwamba ni mbinu mbadala zitakazowasadia maafisaelimu kata, kusimamia kwa karibu suala la kusoma, kuandika na kuhesabu ili watoto wanaohitimu darasa la saba waweza kufaulu mitihani yao ya ndani na hata ya kitaifa.

Aidha, anapongeza juhudi za serikali katika kuinua ubora wa elimu hapa nchini pamoja na walimu huko shuleni, kwani mpango umeishaanza kuzaa matunda, kwani watoto wanaohitimu shule wengi wao wanaweza kusoma, kuandika na hata kuhesabu; ilikilinganishwa na miaka mitano iliyopita.

Amewaonya Maafisaelimu Kata wanaokwenda kuzitumia pikipiki hizo, kwamba vitendeakazi hivyo ni mali ya serikali si mali binafsi; hivyo hategemei kukuta vinafanyakazi kinyume na malengo na maelekezo ya serikali.

Akifafanua jinsi usafiri huo utakavyowasaidia katika utendaji kazi wao, Afisaelimu Kata ambaye jina lake limehifadhiwa, alisema kwamba pikipiki hizo si msaada kwa watoto wa shule za msingi, tu bali hata katika majukumu mengine katika kukuza ubora wa elimu nchini.

Amesema pamoja na kufuatilia suala la KKK, bado atakuwa na nafasi ya kufuatilia masuala ya elimu, aliyoyataja kuwa ni maandalio ya masomo, mahudhurio ya wanafunzi na utendajikazi wa walimu katika shule za msingi na za sekondari katika kata zao.

“Itakuwa ni ajabu nifike shuleni nifanye jambo moja la KKK, wakati shuleni hapo kuna matatizo mengine, au nishindwe kufuatilia utendajikazi wa walimu katika shule ya sekondari ilipo katika kijiji hicho hicho.” alisema Afisaelimu kata huyo.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa