• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

SEQUIP KUWANOA WALIMU 40,000 WA MASOMO YA SAYANSI NA HISABATI - KAGERA

Wakati ilipowekwa: January 6th, 2025

NGARA UPDATES

6/01/2025

Serikali kupitia Mradi wa Mradi wa Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) imeendelea kutoa mafunzo kwa walimu wa sekondari wanaofundisha masomo ya sayansi na hisabati 40,000 ili kuwapatia mbinu, maudhui na matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji shuleni.

Mradi wa SEQUIP unatekelezwa kwa pamoja kati ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na unalenga  kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia katika shule za sekondari kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita kwa muda wa miaka mitano kuanzia 2021 hadi 2026.

Akifungua mafunzo hayo ya siku tano kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Atupele Ambwene katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera leo Januari 6, 2025, Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu na Usimamizi wa Elimu Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Emmanuel Shindika amesema mafunzo hayo yataimarisha mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji wa masomo ya sayansi kwa wanafunzi na walimu pamoja na Wathibiti ubora kufanya tathmini ya masomo hayo nchini.

Amefafanua kuwa hadi kufikia mwezi Desemba 2024, jumla ya walimu 29,328 wamekwishapatiwa mafunzo hayo na katika awamu hii jumla ya walimu 7,940 Wathibiti ubora wa shule 159 kutoka katika mikoa 18 ya Tanzania Bara watapatiwa mafunzo hayo.

Naye, Afisa Elimu Mkoa wa Kagera, Michael Ligola akitoa maelezo ya awali amewaasa washiriki kuzingatia mafunzo wanayopewa ili yakawasaidie katika ufundishaji na tathmini huku akieleza kuwa kwa mwaka 2024 Mkoa huo umeongeza kiwango cha ufaulu ambapo kidato cha sita ufaulu ulikuwa asilimia 100, kidato cha nne (82%), kidato cha pili (72%), darasa la saba (72%) na darasa la nne (84).

Awali, Mratibu Msaidizi Mradi wa SEQUIP,  Richard Makota amesema matarajio  ya mafunzo ni kuwa na ufaulu mzuri wa masomo ya sayansi na hisabati, kuongeza matumizi ya TEHAMA shuleni katika ufundishaji na ujifunzaji, kuongezeka kwa umahiri wa mwalimu katika masomo hayo na ongezeko la wanafunzi katika elimu ya sekondari ya juu, vyuo vya kati na elimu ya juu katika masomo yanayoambatana na sayansi na hisabati.




Ngaradc.go.tz

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa