• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Serikali Iruhusu Akaunti Maalumu kwa Ajili ya Vikundi vya Wanawake na Vijana

Wakati ilipowekwa: October 5th, 2018

Serikali imeombwa kuziruhusu Halmashauri kuongeza akaunti maalumu itakayotumika kutunza fedha za vijana, wanawake na walemavu, ili kurahisishsa shughuli za ukopeshaji na urejeshaji wa fedha hizo.

Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Bi. Josephine J. Rusatira ametoa rai hiyo Septemba 03, wakati alipokuwa akikagua vikundi vya vijana, wanawake na walemavu katika kata za Mabawe, Ntobeye na Rulenge.

“Ofisi ya Maendeleo ya Jamii itaweza kuratibu vizuri shughuli zake na kuweza kujua kwa urahisi madeni na faida, vikundi vinavyodaiwa na vimerejesha kiasi gani, ikiwa serikali itaruhusu kuwepo kwa akaunti maalumu kwa ajili hiyo.” alisema Bi Rusatira.

Amesema ofisi yake inapata shida hata jinsi ya kuwawajibisha wanavikundi wasiotii taratibu za kuresha fedha waliokopa, kwa sababu mikataba haielezi wasiorejeshwa watawajibishwaje.

Ameomba kiongezeke kipengele cha kuvichukulia hatua za kisheria vikundi vyote, ambavyo vitashindwa kurejesha mikopo kwa wakati, na kuongeza kwamba baadhi wanakataa kurejesha kwa kujua kwamba hakuna hatua dhidi yao.

Katika kipindi cha mwaka 2018/2019 ofisi yake itaendelea kukopesha na kufanya ufuatiliaji kwa vikundi vya akina mama na vijana, ambavyo vinasuasua katika kurejesha mikopo yao, ili kubaini matatizo na kuyatafutia ufumbuzi.

kadili ya afisa huyo kitendo cha wankikundi kukopa na kutorejesha kwa wakati kinawakwamisha wanavikundi wenigne wasiweze kukopa, hivyo wanakwamisha lengo la serikali la kutaka kuinua uchumi wa wanawake na vijana.

Aidha, amesema ofisi yake itaboresha mifumo ya ukusanyaji mapato, ili kuongeza kipato na kuweza kutoa asilimia 10% ya mikopo ya vikundi vya wanawake, vijana na walemavu kama ilivyoratibiwa na serikali.

Halmashauri ya Wilaya ya Ngara imekuwa ikitoa mikopo kwa vikundi vya vijana na wanawake, kwa kutumia asilimia 10% ya makusanyo yake ya ndani, ili kuviwezesha kujikwamua kiuchumi na kuutokomeza umasikini uliokithiri katika jamii.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa