• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

WAFANYIKA MKUTANO WA WADAU KUJADILI UTEKELEZAJI MRADI WA UBORESHAJI USALAMA WA MILKI ZA ARDHI WILAYANI NGARA

Wakati ilipowekwa: April 5th, 2024

Leo tarehe 05 April 2024.

Umefanya Mkutano wa wadau kujadili utekelezaji Mradi wa uboreshaji usalama wa milki za ardhi katika Ukumbi wa St Francis Ngara mjini, Ambapo Mgeni Rasmi katika mkutano huo alikuwa  Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Hajjat Fatma Abubakari  Mwassa kauli mbiu ikiwa ni " USAWA WA KIJINSIA KATIKA UMILIKI WA ARDHI KWA USTAWI WA JAMII"

Taarifa fupi ya mradi wa uboreshaji usalama wa milki za ardhi ilisomwa na  Ndg Remigius kawishe Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya.

Katika mkutano huo Mhe. Vitalisi alitoa shukuran kwa Rais Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan pamoja na Mbuge wa Jimbo la Ngara Mhe. Ndaisaba J. Ruholo kwa kutambua umuhimu wa uboreshaji usalama wa milki za ardhi.

Ilitolewa nafasi Kwa wenyeviti wa mitaa mbalimbali kutoa ushuhuda wa Mpango huo na baada ya ushuhuda.

Ripoti ya uwasilishaji wa utekelezaji Mradi halmashauri ya wilaya ya Ngara ilisomwa na msimamizi wa mradi - LTIP, mwakirishi wa wizara ya ardhi pamoja na Meneja uendeshaji mradi vijijini, Ikielezea mradi wa uboreshaji usalama wa milki za ardhi wilaya ya Ngara, Ikiwa ni mipango ya kamati ya ardhi ikiwa ni pamoja na

  • Kuongeza usalama wa matumizi bora ya ardhi
  • Kuboresha miundominu wezeshi za ardhi.
  • Kuanzisha vyuo viwili vya ardhi
  • Kuboresha miundombinu itakayoendana na Teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA).

Msimamizi wa mradi - LTIP ndugu cosmas alimalizia Kwa kutoa shukuran kwa Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Kwa kuleta fedha katika halmashauri ya wilaya ya Ngara zilizowezesha mradi huo.

Wasilisho kutoka Kwa wadau - TANAPA, lilielezea kuwa changamoto ya wanyamapori imeongezeka Kwa sababu Kuna ongezeko kubwa la mifugo ndani ya hifadhi, kuwepo Kwa makazi ndani ya hifadhi, wananchi kutokujua Sheria ya hifadhi, pia matukio ya Rushwa Kwa watumishi pamoja na wananchi ndiyo sababu kubwa inayofanya wanyamapori kuongezeka kutoka kwenye hifadhi na kukimbilia kwenye makazi ya watu na kuleta mahafa kwenye jamii.

 Pia Mdau wa TANAPA Amesema kuwa kumekuwepo na ongezeko kubwa la kipato kupitia utalii, ikiwa ni kupata wawekezaji wapya kwenye miradi ya utalii, lakini pia alitoa gharama za kuingia kwenye hifadhi ikiwa ni kwa mtu mzima ni Tsh. 5900/ Kwa mtoto ni Tsh. 2000/= kama kuna usafiri unalipiwa gari ndogo Tsh. 20000/= na gari kubwa ni Tsh. 40000/=.

Mwisho Amesema kuwa angalau Kwa miezi kumi ameweza kupunguza uvamizi wa hifadhi za taifa ili kulinda ongezeko la wanyamapori kwenye hifadhi hizo pia ametoa shukuran kwa serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan Kwa kuleta miradi inayolinda hifadhi za wanyamapori.

ilitolewa nafasi ya majadiliano Kwa wadau walihudhuria na  maswali yote yaliyoulizwa yalijibiwa Kwa kutolewa  ufafanuzi wa kina na kuwafanya wadau kuridhika, lakini pia wadau walitoa maoni mbali mbali kuhusu mradi wa uboreshaji usalama wa milki za ardhi wilayani.


 Baada ya majadiliano iliazimiwa kwenye mkutano kama ifuatavyo

  1. Elimu kuhusu utekelezaji wa mradi. Wizara pamoja na halmashauri ziendele kutoa elimu.
  2. Utatuzi wa Migogoro,, viongozi Kata wawekeze kutatua migogoro ya ardhi inayojitokeza katika maeneo yao.
  3. Ushirikishwaji wa watendaj wa kata, kushirikishwa katika vikao Vya uendeshaji wa miradi. 
  4. Madiwani na watendaji Kwa kushirikiana na TANAPA, watenge maeneo ya bustani ya wanyamapori (ZOOM). TANAPA watoa ahadi ya kutoa ushauri.
  5. Ardhi ya akiba ya dharura au maafa.
  6. Hakikisheni Sheria za ardhi zinafatwa vizuri, kufanya matumizi yaliyopangwa na sekretereti.
  7. Wanakamati wa mipango watoe taarifa ya matumizi bora ya ardhi, serikal itoe mkazo wa ufatiliaji wa matumizi ya ardhi.

Mwisho imetolewa shukuran Kwa wadau wote waliohudhuria Mkutano ambapo Makamu mwenyekiti wa Halmashauri  Mhe Adronizi Bulindori alifunga Kwa kutoa shukrani  kwa Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe Hajjat Fatma Mwassa pamoja na kamati nzima ya ardhi Kwa kutambua umuhimu wa Mradi huu.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe Hajatt Fatma Mwassa akiwa katika picha ya pamoja  na Mhe Mkuu wa wilaya Col  Mathias Kahabi ,Mkurugenzi Mtendaji Wilaya Ndg Solomon kimilike, Mkiti wa CCM Cde Vitaris Ndailagije, Mkiti wa Halmashauri Mhe Wilbard Bambara katika Ukumbi wa St Francis Ngara Mjini.












Ngaradc.go.tz

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa