• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

DC KANALI KAHABI AFANYA UKAGUZI WA MIRADI WILAYANI NGARA KAGERA

Wakati ilipowekwa: January 13th, 2024

Mkuu wa wilaya Mhe  Kanali Mathias Kahabi amefanya ziara Tena kukagua ujenzi wa Soko la Kahaza na kazi inaendelea  baada ya Mkandarasi kukaa ndani siku mbili Kwa kuonekana Kasi  ya ujenzi wa Soko hilo la Kimkakati kusua sua.

Ukaguzi wa mwanzo alioufanya Mhe Col. Mathias Julius Kahabi Mkuu wa wilaya ya Ngara akifuatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndg Solomon Kimilike, Kamati ya Usalama ya Wilaya, Wasimamizi wa Mradi LADP, Wataalam wa Halmashauri chini ya Mkurugenzi Mtendaji, Mkandarasi pamoja na Viongozi wa Serikali ya kijijni cha Rusumo tarehe 23/12/2023.

Ambapo hawakuridhishwa na Maendeleo ya Ujenzi wa mradi huo  Mhe Mkuu wa wilaya Col. Kahabi alilazimika kumuweka ndani Mkandarasi kwa kushindwa kwenda na kasi inayotakiwa kulingana na Mkataba ambapo alikuwa ameshalipwa TShs Milioni 377 kama malipo ya awali (Advance Payment). 

Aidha Pamoja na malipo hayo ya awali Mkandarasi hakuweza kwenda na kasi inayotakiwa ikiwemo kushindwa kuleta local and industrial materials ya kutosha kwenye eneo la mradi.

Baada ya ukaguzi huo Mkandarasi huyo alifanya commitment mwenyewe kwa Mkuu wa Wilaya Mhe kanali Kahabi na Kamati ya Usalama ya Wilaya kwamba atahakikksha mradi unaenda kwa kasi kubwa na kwamba atamaliza Ujenzi wa mradi huo ifikapo mwezi March 2024 kama ilivyo kwenye Mkataba.

Leo tarehe 13/01/2024, Mhe Col Mathias Kahabi ametembelea mradi huo akifuatana na Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Usalama ya Wilaya, Wataalam wasimamizi wa mradi LADP, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, Mkandarasi pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali ya kijijni cha Rusumo na kuridhishwa na kasi inaendelea hivi sasa na Materials yaliyopo site, hivyo ameagiza kasi iendelee na kwamba yeye na Viongozi wenzake watakuwa wanafika angalau mara mbili kwa wiki kwa ajili ya ukaguzi wa Ujenzi wa mradi huo.

Aidha Mkuu wa Wilaya Mhe Kanali Kahabi  amesema kamwe  hatakubali kuona Juhudi kubwa za Mhe Dr. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  zinajaribu kuchafuliwa na Wakandarasi wachache wanaotaka kumrudisha nyuma Mhe Rais. Soko hilo linatarajiwa kukamlika mwezi March 2024.

Pia Mhe Mkuu wa wilaya na timu yake wametembelea Mradi wa ujenzi wa bweni, Bwalo na jengo la utawala  shule ya sekondari Ngara high school.


Mafundi kazi ya ujenzi wa soko Mkakati la kahaza Rusumo Wilayani Ngara ambapo Mhe Mkuu wa wilaya alifuatana na Mkurugenzi Mtendaji Ili kuona hali ya ujenzi.



Mafundi kazi ikiendelea.


Mafundi  kazi ikiendelea  soko Mkakati kahaza Kata ya Rusumo Wilaya ya Ngara.




Mhe col Mathias Kahabi Mkuu wa wilaya (mtu kazi )akiwa na kamanda wa Polisi Wilaya, Mtendaji wa Kijiji  wakikagua ujenzi.


Mkuu wa wilaya Col. Kahabi akiwa na kaimu katibu Tawala Ndg Jawadu Yusuf, kamanda wa Polisi Wilaya,Mtendaji wa Kijiji,na  Maafisa Toka LADP.


Mhe Kanali Mathias J Kahabi akiwa na viongozi mbalimbali katika ujenzi wa bweni shule ya Sekondari Ngara high school.


Mhe Kanali Mathias J Kahabi akiwa na viongozi mbalimbali katika ujenzi wa bweni, Bwalo na jengo la utawala  shule ya Sekondari Ngara high school (Mradi unaosimamiwa na LADP).


Mhe col. Kahabi akipata maelezo mbalimbali ya ujenzi wa bweni , Bwalo na jengo la utawala shule ya Sekondari Ngara high school.


Mhe Col. Kahabi akiwa eneo la ujenzi.


Mhe Mkuu wa wilaya amesisitiza vifaa vyote vya ujenzi viwepo site  bila kukosa kwenye ujenzi wa soko la kahaza Rusumo Wilayani Ngara.

ngaradc.go.tz

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa