• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Halmashauri Yapokea Zaidi ya Milioni 300 za Kujenga Miundombinu: Mwesiga

Wakati ilipowekwa: May 16th, 2019

Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R) imeipatia shilingi 321,938,000.00, Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, kama fedha ya motisha kwa kujaza takwimu za mwaka 2018 na kukidhi vigezo, zitumike katika ujenzi wa miundombinu shule za msingi na sekondari.

Haya ameyasema Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara na Afisaelimu Ndugu Gideon Mwesiga, wakati wa kikoa cha wataalamu (CMT) Mei 15, 2019, wakati akiwakirisha mapokezi ya fedha hiyo katika kikao hicho.

“Idara ya Elimu Msingi na Sekondari tumepokea fedha hiyo, na katika barua ya katibu Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), yenye Kumb. Na. DB, 291/298/3/47 ya Mei 10, 2019 imeelekeza matumizi ya fedha hiyo.” Alisema Ndugu Mwesiga.

Kadiri ya barua, asilimia 50 ambazo ni sawa na shilingi 160,969,000.00 zitatumika katika kukamilisha maboma na ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule za msingi, ambapo asilimia 50 ya fedha hiyo, imeingizwa moja kwa moja katika akaunti za shule zilizopata ufadhili huo.

Barua hiyo, imelekeza kuwa asilimia 20 sawa na shilingi 64,387,600.00, zitatumika kupanga ikama katika shule za msingi na za sekondari, ambapo asilimia 10 sawa na shilingi 32,198,800.00 zitatumika katika shule za msingi; huku asilimia 10 sawa na shilingi 32,198,800.00 itatumika kupanga ikama katika shule za sekondari.

Imeagizwa kwamba katika asilimia 10 ya fedha iliyotumwa ambayo ni sawa na shilingi 32,198,800.00; idara ya Elimu Msingi itatumia shilingi 16,096,900.00 katika ufuatiliaji na tathimini katika shule za sekondari na shilingi 16,096,900.00 kwa ajili ya shule za msingi,

Ndugu Mwesiga ameongeza kwamba barua hiyo imeagiza kwamba asilimia 10 sawa na shilingi 32,198,800.00; Idara ya Elimu Msingi itatumia kiasi cha shilingi 16,096,900.00, na idara ya Elimu sekondari shilingi 16,096,900.00 kwa ajili ya ukusanyaji wa takwimu.

“Tunaweza kusema kwamba Idara ya Elimu Msingi katika fedha ya motisha tumepata jumla ya shilingi 257,550,400.00 sawa na sasilimia 80, huku Idara ya Elimu Sekondari ikipata shilingi 64,387,000.00 sawa na asilimia 20 ya fedha iliyopokelewa kutoka program ya Lipa Kulinga na Matokeo (EP4R).” Alisema Ndugu Mwesiga.

Aidha, ameishukuru serikali kwa kuleta fedha hiyo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, kwa kudai kwamba itapunguza changamoto za miundombinu katika shule hizo; huku akiishukuru kwa kuwapanga walimu 37 katika katika Halmashauri hiyo katika ajira mpya ya mwaka 2018/2019, ambapo kati yao walimu 06 pekee hawajalipoti katika vituo vyao.

Hata hivyo, Ndugu Mwesiga amefafanua kuwa kiasi cha fedha kilichopokelewa kimeshuka kutoka zaidi ya shilingi milioni 500 zilizopokelewa mwaka wa fedha wa 2017/2019 na kufikia zaidi ya shilingi milioni 300 katika mwaka wa fedha wa 2018/2019.

akifafanua sababu ya upungufu huo; amesema kwamba mwaka 2018 zaidi ya walimu 200, wamehama kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, na kusababisha ikama katika Idara za Elimu Sekondari na Msingi kupungua, kitendo kilichopelekea idara hizo kupata fedha pungufu, ikilinganishwa na fedha iliyotolewa mwaka 2017/2018 wa fedha.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa