• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Kamati za Ukimwi Zahimizwa Kuwahamasisha Wananchi Kupima Afya Zao

Wakati ilipowekwa: December 3rd, 2018

Kamati za Ukimwi Mkoani Kagera zimetakiwa kuwahamasisha na kuwahimiza wananchi waendelee kupima Virus vya Ukimwi, kwa lengo la kujua afya zao. ili wajiepushe na maabukizi ya ugonjwa huo.

Haya ni kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Ngara Lt. Col. Michael Mntenjele, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brig. Jen. Marco Elisha Gaguti katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani, iliyosherehekewa Kimkoa Wilayani Ngara Desemba 01, 2018.

“Wananchi tujitokeze kupima afya zetu, tukilenga kufikia lengo la Dunia la90% ya watu wote wawe wamepime virus vya ukimwi, 90% ya watu wawe wanatumia ARV, na 90% watu wawe wamefubaza virus vya ukimwi ili wawsiwe na uwezo wa kuambukiza.” Alisema Lt. Col. Mntenjele.

Lt. Col. Mntenjele amesema kwamba kamati zinawajibika kutoa elimu na hamasa kwa wananchi, ili kwa hiari yao wakapime virus vya ukimwi, kwa madai kwamba wakishajua afya zao, watajilinda kwa kufuata maelekezo ya wataalamu.

Amezitaka kamati za ukimwi kushirikiana na mashirika yanasaidiana na serikali kuthibiti kuenea kwa virus vya ukimwi, kuwaelimisha wananchi wajitokeze kwa hiari kupima virus vya kwa lengo la kudhibiti gonjwa hili hatari.

Aidha, amesema kitaifa takwimu zinaonyesha kwamba Januari – Oktoba 2018; watu 1,291,735 walipima virus vya ukimwi, kati yao 16,048 sawa na 1.2% walikuwa wameambukizwa virusi vya ukimwi, ikilinganishwa na Januari – Desemba 2017 ambapo maambukizi yalikuwa 1.6%.

Katika Mkoa wa Kagera takwimu zinaonyesha kuwa maambukizi tangu Januari hadi Oktoba 2018; Wilaya ya Missenyi ilikuwa na 1.8%, Ngara 0.5%, Muleba 1.7%, Bukoba Manispaa 1.7%, Bukoba Vijijini 1.7%, Kyerwa 1.2%, Biharamulo 1.0 ambapo Karagwe maambukizi yalikuwa 1.0%.

Amewakumbusha wananchi wa Wilaya ya Ngara wasijivune kwa takwimu hizo, kwani wanopima afya zao ni wale wanaojiamini, huku akisdai kwamba wasiopima ni wale wenye mashaka na afya zao; kwa hiyo, mtu atajua yuko salama au la kwa kupima na si vinginevyo.

Wakti huo huo, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Amani Anasitazi Mpanju, amesema maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani, yanaagukia katika siku 16 zinazolenga kupinga ukatili dhidi ya wanawake, watoto na makundi mengine katika jamii.

“Nimejumuika katika maadhimisho haya, kwa sababu tunapoongelea kupinga ukatili dhidi ya ya makundi ya wanawake, watoto na wengine katika jamii yetu, hatuwezi kukwepa sekta ya sheria, ambayo wizara yangu ndiyo yenye dhamana.” Alisema Ndugu Mpanju.

Wizara ya Katiba na Sheria inaelekezwa kuhakikisha makundi ya pembezoni, ikiwemo watu wanaoishi na virus vya ukimwi, wanapata huduma ya msaada wa kisheria, ili waweze kupata haki zao pasipokuwa na vikwazo vyovyote.

Amesema yapo makundi kwa muda mrefu wamekuwa hawapati haki zao, kwa sababu ya gharama za kuwalipa mawakili waweze kupata haki, na moja ya makundi hayo ni watanzania wanaoishi na virus vya ukimwi.

Kilele cha maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani yamefanyika kimkoa Wilayani Ngara na kuhudhuliwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Ndugu Amani Anastazi Mpanju, Mganga mkuu wa Mkoa wa Kagera Dr. Marco Mbata, Mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na viongozi wa wilaya ya Ngara.

Pia Maadhimisho hayo yamefutia wananchi kwa hiari kupima afya zao, kupata ushauri nasaha, wa kisheria na hata kufanya tohara kwa vijana na wanaume wenye umri wa miaka 18 na kunedelea; ambapo Kauli mbiu ya katika maadhimisho hayo inasema; “Pima, Jitambue, Ishi.”

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa