• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Kazingati Wataka Serikali Imruhusu Mwekezaji wa Korea Awekeze Kijijini Kwao

Wakati ilipowekwa: January 3rd, 2019

Wananchi wa Kijiji cha Kazingati kata ya Keza katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara wameiomba serikali imruhusu mwekezaji toka nchini Korea Kusini awekeze kijijini humo, ili waweze kunufaika na ajira pamoja na tecknolojia ya kilimo cha kahawa na mpunga itakayokuja na mwekezaji huyo.

Wananchi hao wameyasema hayo wakati wakiongea na Mbunge wa Jimbo la Ngara Mkoani Kagera Mh. Alex Gashaza (CCM) wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Kazingati Januari 02, 2019 baada ya kuwepo malalamiko ya kwamba anapinga wawekezaji kupata ardhi kijijini humo.

Katika mkutano huo wananchi wamepinga hoja ya Mbunge kwamba, haukufuatwa utaratibu wa kugawa ardhi ya kijiji hicho kwa wawekezaji kutoka Korea Kusini; “tuliitwa na Mwenyekiti wa kijiji, akatuuliza kuhusu kutoa ardhi yetu kwa mwekezaji wa Korea Kusini tulimkubalia tukitarajia kupata ajira.” Alisema Ndugu Daniel.

Wamesema kwamba wanaridhia wawekezaji wa taifa hilo, kuanzisha miradi ya maendeleo kijijini kwao, wajipatie ajira ili wajikwamue kiuchumi; huku wakidai ardhi iliyopo ni maeneo ya wazi hawanufaiki nayo ukiachilia mbali watu wasiowanakijiji kuyafanya malisho ya mifugo.

“Sisi wananchi wa kijii cha Kazingati tunamtaka mwekezaji toka Korea Kusini, ili tupate ajira na kunufaika na teknolojia mpya itakayokuja na mwekezaji huyo, kwani ardhi iliyopo katika kijiji hiki inatosha kuwekeza; wewe unapinga wawekezaji lini tutapata ajira na kufaidika?” Alihoji mmoja wa wananchi wa kijiji hicho Ndugu Mathayo Daniel.

Ndugu Daniel amesema ardhi hiyo imejaa ng’ombe wanaotoka kwa wafugaji wa nje ya kijiji hicho, lakini wananchi wa kazingati hawanufaiki ispokuwa viongozi; huku akitaka wawekezaji hao waruhusiwe kuanzisha miradi yao katika ardhi hiyo.

Mbunge wa Ngara Mhe.Alex Gashaza anapinga kutolewa ardhi kwa wawekezaji wa Korea Kusini baada ya kusainiwa mkataba (MOU) wa kupewa ardhi ekari 12,000 wakati na wananchi wa Kazingati wameridhia.

Aidha madai ya Mbunge huyo ni kwamba hakuna kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara kilifanyika kupitisha kugawa ardhi ya kijiji cha Kazingati ambayo ilibainishwa kwenye vitongoji vya vya Muko na Msalasi vyenye ukubwa usiozidi ekari 4,140.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ngara,Mhe. Erick Nkilamachumu amesema, utaratibu wa kutoa ardhi ulifuatwa na malengo ni wananchi kupata miradi ili waweze kujiinua kiuchumi, na si vinginevyo.

Amesema matarajio ya Halmashauri ilikuwa kupata wawekezaji kuunga mkono juhudi za serikali ya Tanzania kuwa na uchumi wa kati wa viwanda, ambapo hata Wilaya ya Ngara ingesonga mbele kwani wawekezaji hao wangelipa mapato

"Mgogoro huo hadi Halmashauri iufikishe Wizara ya Ardhi kwa Waziri mwenye dhamana ndiye atakayeweza kuutolea ufafanuzi badala ya kujibia hoja mkanganyiko nisijichonganishe na wananchi ".Amesema Nkilamachumu

Mbunge huyo Gashaza amefanya mkutano huo January 2, 2019 ikiwa ni siku chache baada ya Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi ngazi ya Taifa kuagiza uongozi wa wilaya ya Ngara kuacha mara moja mipango ya kugawa ardhi kwa mwekezaji kutoka korea Kusini.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa