• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

MHE.KAHABI -DC AFANYA ZIARA KUTEMBELEA BARABARA YA MURUNYINYA HADI KUMUYANGE NA MRADI WA MAJI KIGINA/KUMUYANGE WILAYANI NGARA

Wakati ilipowekwa: December 27th, 2024

NGARA UPDATES

27/12/2024

Mhe. Col Mathias J Kahabi  Mkuu wa Wilaya ya Ngara amefanya ziara kukagua barabara ya Kumuyange – Mugasha – Murunyinya yenye urefu wa KM. 13.3 pamoja na Mradi wa maji wa Kumuyange Kata ya Nyamiaga na Kigina Kata ya Ntobeye.

Katika Ziara hiyo ameambatana na Afisa Tarafa Nyamiaga Bw. Jawadu Yusuph, Kaimu Meneja wa TARURA Bw. Emmanuel ndalihaze, na Afisa Mtendaji wa Kata ya Murukulazo Bw. Julian mwesiga. Kutoka Ofisi ya Meneja wa RUWASA Wilaya ya Ngara aliambatana na Bw. Rashid Omar Mwalimu na Bw. Innocent Medard Kahaya.  

kwa upande wa Barabara ya Murunyinya hadi Kumuyange yapo maeneo ambayo yameharibika na yanahitaji matengenezo hususani kipande cha Barabara kuanzia Murunyinya hadi shule ya msingi Bulengo.

Kaimu Meneja wa TARURA amemueleza Mhe. Col Kahabi Mkuu wa Wilaya kuwa katika mwaka wa fedha 20224/2025 TARURA Wilaya ya Ngara kupitia fedha ya Mfuko wa Jimbo iliingia Mkataba na Mkandarasi Chomola Technical (T) Ltd Mkataba na. 510/006/2024/2025/W/22 kutengeneza matengenezo ya kiwango cha changarawe urefu wa KM. 2 kwa gharama ya Tshs. 42,715,500.00 katika matengenezo haya eneo litakalotengenezwa ni kuanzia Shule ya Msingi Mugasha hadi kwenye senta ya Chamukube.

Ameeleza pia Katika mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 TARURA Wilaya ya Ngara imetenga pia kiasi cha Tshs. 25,000,000.00 kupitia bajeti za fedha za Mfuko wa Jimbo itatengeneza kipande cha urefu wa KM. 1 kwa kiwango cha changarawe na kujenga Calvati moja eneo ambalo Barabara imekatika.

Baada ya bajeti kupitishwa  Ofisi ya TARURA itapita tena kwenye Barabara hiyo ili kubaini maeneo ambayo yameharibika kwa ajili ya kufanya makisio ili yaweze kutengenezwa.

Kwa upande wa Mradi wa maji Kumuyange/ Kigina amekagua utekelezaji wa Mradi huo unaotekelezwa na Mkandarasi Buzubona & Sons Co. Ltd kwa thamani ya Tshs. 1,669,188,309.52. Utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 20 na unatarajiwa kukamilkika ifikapo tarehe 10/03/2025.  Aidha kukamilika kwa Mradi huu utawanufaisha Wananchi wapatao 2000 wa Kitongoji cha Kumuyange.  

Shughuli zilizotekelezwa mpaka sasa ni ujenzi wa chanzo, Ujenzi wa tenki lita. 25,000 na ujenzi wa tenki lita 75,000 pamoja na kuchimba mtaro wa urefu wa 10.8 KM na utajumuisha kuunganisha maji majumbani kwa Kaya 50 pamoja na ujenzi wa vituo viwili vya kuchotea maji kwa upande wa Kumuyange.

Kwa upande wa Kigina shughuli zitakazotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa chanzo, tenki lita 25,000, tenki lita 50,000, tenki lita 120,000 pamoja na ujenzi wa nyumba ya Mitambo (Pump House), Ufungaji wa mfumo wa umeme jua,  Ufungaji wa “Pump” ya kusukuma maji, kuchimba mtaro na kulaza bomba  26.6 KM pamoja na kuunganisha maji majumbani kwa kaya 100.

Katika Ziara hiyo Mhe Col Kahabi Mkuu wa Wilaya ameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Mradi huo pamoja na kumpongeza Mkandarasi na ameiagiza Ofisi ya Meneja RUWASA kumsimsmia Mkandarasi ili akamilishe utekelezaji wa Mradi huo kwa wakati ili Wananchi wapate kunufaika na mradi huo.

Mhe Col Kahabi Mkuu wa Wilaya ameagiza pia Meneja wa RUWASA kutembelea Kitongoji cha Songambele Kijiji cha Nterungwe ili kutatua changamoto ya ukosefu wa Maji katika Kitongoji hicho.





Kazi inaendelea 

www.ngaradc.go.tz

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa