• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Ongezeni Miundombinu Tukidhi Idadi Kubwa ya Wanafunzi; Ndugu Mwesiga

Wakati ilipowekwa: January 15th, 2019

Wazazi wote katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, wametakiwa kuhakikisha wanaongeza miundombinu katika shule za msingi na za sekondari, ili waweze kukidhi ongezeko kubwa la wanafunzi wanaojiunga na masomo kila mwaka.

Wito huo umetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Gideon Samson Mwesiga Januari 15, 2019, kwamba uzoefu umeonyesha kila mwaka wanafunzi wanaojiunga darasa awali, la kwanza na kidato cha kwanza wanaongezeka mara dufu.

“Tumejifunza kwamba kadili tunavyoandikisha watoto kila mwaka; ndivyo tunavyopata wanafunzi wengi zaidi na ndivyo mahitaji ya miundombinu yanavyoongezeka, kwa hiyo wazazi wote wanawajibika kuandaa miundombinu hiyo, kusudi tuweze kuwasaidia watoto wetu.” Alisema Ndugu Mwesiga.

Amesema wamejifunza kwamba mpango wa serikali wa elimu bila malipo, limesababisha ongezeko kubwa la wanafunzi katika shule za sekondari na zile za msingi kila mwaka; huku akiongeza kwamba mwaka 2019 tunatarajia kusajili wanafunzi wapatao 21,000 kwa wanafunzi wa darasa la kwanza na awali.

“Wito wangu kwa wananchi tujitahidi kuweka benki ya matofali, mawe na mchanga na halmashauri itaweza kutoa vifaaa vya viwandani, ili tujenge miundombinu kwa ajili ya kuwawezesha watoto wetu kujifunza bila bughudha.” Alishauri Ndugu Mwesiga.

Pia aliwasisitiza wazazi kuwahimiza wanafunzi wahudhulie masomo yao kama taratibu na kanuni za serikali zinavyowataka; huku akiwataka wazazi hao wahakikishe watoto wao kuwapa mahitaji muhimu ili waweze kuyamudu masomo yao.

Akiongelea changamoto, amesema kufikia Desemba 2018; idara ya elimu msingi ilikuwa ina mahitaji ya vyumba vya madarasa vipatavyo 1869; lakini ina upungufu wa vyumba 1059, nyumba za walimu 1207, matundu ya vyoo yapatayo 775, ambapo mapungufu ya ofisi za walimu ni 251.

Hata hivyo, amesema idara ya elimu msingi ina mapango wa kutumia mapato ya ndani, kugharimia vifaa vya viwandani, kwa ajili ya kusapoti nguvu za wananchi, ili kuondoa kabisa tatizo la upungufu wa madarasa.

Pia, idara kwa kushirikiana na Mh. Mbunge wa Jimbo la uchaguzi la Ngara, watachangia ujenzi wa miundombinu kupitia mfuko wa jimbo; pamoja na kuendelea kuweka kwenye bajeti maombi ya fedha za ujenzi wa miundombinu hiyo.

Aidha, amesema kupitia mradi wa Local Area Development Program (LADP) Halmashauri itajenga vyumba vya madarasa 10, majengo ya utawala 02, nyumba za walimu 02, matundu ya vyoo 24, pamoja kutengeneza madawati na viti ingawa idfadi kamili haijajulikana katika shule za Mgoma na Mkugwa.

Ameishukuru serikali kwa jitihada inazozifanya kwani tangu Julai hadi Novemba 2018 idara ya elimu msingi, imepokea shilingi 316, 426,000.00 kwa ajili ya elimu bila malipo; rusuku ya uendeshaji wa shule 173,926,000.00; posho ya madaraka kwa walimu wakuu 115,000,000.00 pamoja na 27,500,000.00 kwa ajili ya posho ya maafisaelimu kata.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa