• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

RAIS DKT. SAMIA: TUZO YA CAF INANIPA NGUVU YA KUANDAA AFCON 2027

Wakati ilipowekwa: January 10th, 2026

Rais Samia Suluhu Hassan amesema tuzo aliyotunukiwa na Rais wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Dkt. Patrice Motsepe, imempa nguvu na motisha zaidi ya kuandaa kwa ufanisi Mashindano makubwa ya soka kwa Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2027, yatakayoandaliwa kwa pamoja na Kenya na Uganda.

Akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha mchana aliyoiandaa kwa ajili ya wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) pamoja na wanamichezo wengine waliofanya vizuri katika michezo mbalimbali, Rais Samia amesema tuzo hiyo ni heshima kubwa na imempa hamasa ya kuhakikisha maandalizi ya michuano hiyo yanafanyika kwa kiwango cha juu.

Ameongeza kuwa tuzo ya kutambua mchango wake katika kukuza mchezo wa soka nchini ni chachu kwa Tanzania kufanya vizuri zaidi siyo tu katika soka, bali pia katika michezo mingine.

Ikumbukwe pia kuwa Novemba 19, 2025, Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) lilimtunuku Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Kenya William Ruto na Rais wa Uganda Yoweri Museveni tuzo ya heshima kwa mchango wao katika kuandaa kwa mafanikio michuano ya CHAN.


RAIS DKT. SAMIA: WALIOTAKA KUVURUGA AMANI NA KUCHAFUA SIFA YA TAIFA LETU WASHINDWE NA WALEGEE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema amepokea tuzo tatu za kimataifa akiwa Zanzibar, ikiwa ni matokeo ya juhudi za serikali katika kulinda amani, kuimarisha utalii na kutangaza taswira chanya ya nchi.

Rais Samia amesema Tanzania imepewa kikombe cha kutambuliwa kama nchi bora ya utalii barani Afrika, pamoja na tuzo ya kuwa miongoni mwa nchi bora za utalii duniani. Aidha, Hifadhi ya Taifa ya Serengeti pia imepewa tuzo maalumu kutokana na mchango wake mkubwa katika uhifadhi na kuvutia watalii duniani.

Vilevile, Zanzibar imepokea tuzo ya kutambuliwa kama mji bora wa mikutano ya kimataifa, hatua inayothibitisha hadhi yake katika sekta ya utalii wa mikutano na uwekezaji.

Akizungumzia mafanikio hayo, Rais Samia amesisitiza kuwa tuzo hizo ni ushahidi wa amani, mshikamano na sifa njema ya Tanzania kimataifa. Ameongeza kuwa jitihada zozote za kuharibu amani na taswira ya taifa hazitafanikiwa, akisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kuwa kisiwa cha amani.

“Kwa waliotaka kutuharibia amani na kuichafua sifa ya taifa letu, washindwe na walegee. Tanzania itaendelea kuwa kisiwa cha amani,” amesema Rais Samia.

RAIS DKT. SAMIA: DUNIA IMEONA WAZI TULIPAMBANA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewapongeza wachezaji wa Timu ya Taifa (Taifa Stars) kwa kufanikiwa kufika hatua ya 16 bora ya michuano ya AFCON, akieleza kuwa ni mafanikio makubwa kwa taifa.

Akizungumza leo Ikulu wakati wa chakula cha mchana alichokiandaa kwa ajili ya kuzungumza na timu hiyo, Rais Samia pia aliizungumzia mechi kati ya Morocco na Tanzania, akibainisha kuwa mchezo huo ulikuwa na utata wa hapa na pale.

Rais amesema kuwa Tanzania ilicheza dhidi ya timu mwenyeji na yenye ushawishi mkubwa, akisisitiza kuwa kilichotokea kinaeleweka kutokana na mazingira ya mashindano. Hata hivyo, ameeleza kuwa juhudi na mapambano ya wachezaji wa Taifa Stars yalionekana wazi, si kwa Watanzania pekee bali pia kwa dunia nzima.

“Tulicheza dhidi ya wenyeji, taifa lenye fedha na ushawishi mkubwa kwa waandaaji, lakini tuliona wazi, na dunia imeona wazi, kwamba Tanzania ni wapambanaji na wamepambana,” amesema Rais Samia.

Ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuwaunga mkono wachezaji na sekta ya michezo kwa ujumla, akiwahimiza Taifa Stars kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuiletea nchi heshima katika mashindano yajayo.

RAIS DKT. SAMIA AKABIDHIWA TUZO KUTOKA CAF

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, leo amepokea tuzo ya jezi maalumu kutoka kwa wachezaji wa Timu ya Taifa (Taifa Stars), jezi iliyosainiwa na baadhi ya wachezaji wa kikosi hicho, kama ishara ya heshima na shukrani kwa mchango wake katika maendeleo ya michezo nchini.

Hafla hiyo imefanyika leo Ikulu jijini Dar es Salaam, wakati wa chakula cha mchana, ambapo Rais Samia amekutana na wachezaji, viongozi wa michezo pamoja na wadau mbalimbali wa sekta hiyo.

Aidha, Rais Samia pia amepokea tuzo nyingine kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), ikiwa ni kutambua ushiriki wake na kuunga mkono jitihada za maendeleo ya michezo, hususan mpira wa miguu, ndani na nje ya nchi.

Katika hafla hiyo, viongozi wa michezo wamepongeza uongozi wa Rais Samia kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya michezo, kuimarisha michezo ya vijana, na kuiwezesha Tanzania kushiriki kikamilifu katika mashindano ya kimataifa.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hizo, Rais Samia ameahidi kuwa serikali itaendelea kuwekeza katika sekta ya michezo ili kuibua vipaji, kuongeza ajira kwa vijana na kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia michezo.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • RAIS DKT. SAMIA: TUZO YA CAF INANIPA NGUVU YA KUANDAA AFCON 2027

    January 10, 2026
  • NAIBU WAZIRI DKT. SAMIZI APOKEA MAWASILIANO KUTOKA VITENGO, IDARA NA PROGRAMU ZA WIZARA YA AFYA

    January 10, 2026
  • DKT. MWIGULU ANAZUNGUMZA NA MACHINGA, MADEREVA PIKIPIKI NA BAJAJI

    January 08, 2026
  • SALAMU ZA MWAKA MPYA KUTOKA KWA DED NGARA

    January 01, 2026
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa