• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

SERIKALI YATOA AGIZO KWA MKANDARASI KUKAMILISHA MRADI WA LUSAHUNGA - RUSUMO WENYE DHAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 153

Wakati ilipowekwa: January 12th, 2025

Serikali imeelekeza Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Barabara ya Lusahunga-Rusumo kuhakikisha unakamilika kwa wakati ili kuleta tija kwa wananchi na watumiaji wa eneo hilo. Mradi huo, wenye thamani ya shilingi bilioni 153, unatekelezwa na Kampuni ya China Civil Engineering Construction Cooperation (CCECC), chini ya usimamizi wa makampuni ya Noplan na Tisa. 

Ujenzi wa barabara ya Lusahunga-Rusumo kwa kiwango cha lami, inayounganisha Tanzania na nchi jirani za Rwanda, Burundi, na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, unatarajiwa kukuza uchumi wa Tanzania kupitia sekta ya usafirishaji.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, alibainisha hayo alipokagua maendeleo ya mradi huo. Alisema barabara hii ni kiunganishi muhimu kwa Tanzania na nchi jirani, kwani inatumika kusafirisha mizigo kutoka bandarini, hali itakayochochea uchumi wa taifa na kuboresha maisha ya wananchi.

Hata hivyo, Naibu waziri kasekenya aliwataka wasimamizi na wakandarasi kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo, ambao upo nyuma kwa asilimia 18. Aidha, alisisitiza umuhimu wa kuhakikisha mradi unakamilika kwa viwango vya juu ili kuendana na thamani halisi ya fedha zilizotolewa.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi,Mhandisi George Mwandiga, alisema barabara hiyo itakuwa na urefu wa kilomita 92 na kujumuisha madaraja na makaravati 133. Mradi huo unagharimu zaidi ya shilingi bilioni 153, fedha zinazotolewa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.

Mmoja wa wananchi wanaotumia barabara hiyo, Mussa Abeli Kaleji, ameishukuru serikali kwa hatua hiyo. Pia, amempongeza mkandarasi wa mradi kwa kutoa ajira kwa wakazi wa eneo hilo hatua inayochangia kuboresha maisha yao.

Utekelezaji wa mradi ulianza rasmi tarehe 5 Julai 2024, na unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 5 Julai 2025. Hadi sasa, kazi za ujenzi zimefikia asilimia 20 ya utekelezaji wake. Serikali imesisitiza umuhimu wa kasi ya utekelezaji kuongezwa ili kuhakikisha lengo la mradi linafikiwa kwa wakati uliopangwa.


ngaradc.go.tz


Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa