• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Tumieni Muda Wenu Kufanyatoba na Kujipatanisha na Mwenyezi Mungu

Wakati ilipowekwa: May 2nd, 2019

Wananchi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, wametakiwa kutumia muda wao kufanya toba, kumshukuru Mwenyezi Mungu pamoja na kuishi vizuri na watu wenzao, huku akiwataka kuacha mambo mengine kwa Mungu.

Hayo ni kwa mujibu wa Mchungaji wa Kanisa la Kiluteli la Kikiristo Tanzania Oscar Samwel, wakati wa ibada ya kumuaga aliyekuwa Afisaelimu idara ya sekondari Marehemu Fikeni Ezekiel Senzighe, iliyofanyika katika Kanisa la Kiluteli Wilayani Ngara Mei 01, 2019.

 “Kila mtu ajiadae nafsi yake ili siku mwili ukifa, roho zettu zikapate kibali mbele ya Mungu, mwenzetu ameotangulia, sisi tumshukuru Mungu hata kwa muda mfupi alioishi Ngara.” Alkisema Mchungaji Samwel.

Ameonya kutoyafanyia kazi maswali yanayoweza kujitokeza, kwa sababu ya ubinadamu wetu; kwa kudai kwamba hakuna hata mmoja mwenye majibu sahihi ya maswali hayo, na hata majibu yakiwepo hakuna la kufanya.

Ameyataja maswali hayo; kwanini amekufa wakati kakaa muda mfupi katika ofisi hiyo? alipata ajali juzi, kwa nini kafa kwa ajali kama ile? mbona na dereva waliyekuwa naye alikuwa amepata ajali hivi karibu? na mbona aliyemtangulia katika nafasi hiyo naye alikufa kwa ajali?

Kadiri ya Mchungaji Samwel  maswali hayo yakipewa nafasi yataleta uhasama, chuki na kusababisha watu wakosane bure, wakati inafahamika kuwa maisha ya binadamu hapa duniani si ya kudumu, huku akisisitiza kwamba kila nafsi itaonja mauti.

“Nawakubusha imeandikwa kwamba kila nafsi itaonja mauti; iwe kwa ajali, kuuawa kwa sumu, kukatwakatwa panga, na hata kwa kuugua, bado ni kifo tu; tunalopaswa kufanya ni kujipatanisha na Mungu pamoja na wenzetu.” Alisema mchungaji Samwel.

Aidha, Afisaelimu Mkoani Kagera Ndugu Aloyse Kamamba, amesema marehemu alikaa muda mfupi katika idara ya elimu sekondari, lakini alikuwa msaada sana kwake; kwani walikuwa wakifanya naye kazi kwa karibu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama, ameushukuru uongozi wa wilaya ya Ngara, kwa ushirikiano walionyesha tangu kutokea kwa ajali hadi mauti ya mwenzetu, na kuwataka wahudumishe ushirikiano huo.

Marehemu Senzighe alifariki dunia na wenigne watano kujaruhiwa April 30, 2019,  katika pori la Kimisi Wilayani Karagwe mkoani Kagera, baada ya gari aina ya Landcruser lenye usajili wa Namba STK 6591 kupinduka.

Kamanda Malima amemtaja dereva wa gari hilo kuwa ni Ndugu Stanley, ambapo majeruhi wa ajali hiyo ni Askari Amenya Nestory, aliyepewa rufaha kwa ajili ya matibabu zaidi April 30, 2019 katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando mkoani Mwanza.

Wahanga wengine wa ajali hiyo ni Afisaelimu Vifaa na Takwimu Ndugu Martoni James, Afisaelimu Taaluma Ndugu Gerad Nyahonge pamoja na Jebili Abdallah ambaye ni askair polisi.  

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NGARA YAFANYA VIZURI MICHEZO YA SHULE ZA MSINGI UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA

    May 30, 2025
  • MHE. COL MATHIAS KAHABI DC NGARA AKUTANA NA BALOZI WA RWANDA.

    May 29, 2025
  • NGARA YAENDELEA VIZURI NA MICHEZO YA SHULE ZA MSINGI UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA.

    May 26, 2025
  • MADEREVA WAPATIWA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI ILI KUPUNGUZA AJALI - NGARA

    May 24, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa