• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Ukinunua Kahawa kwa Mkulima Tukakujua Kazi Yetu ni Kukufilisi; Bahama

Wakati ilipowekwa: July 31st, 2018

“Kahawa imezuiliwa kununuliwa na mtu wa kawaida; mkulima anatakiwa aivune, na aiuze kahawa yake kwa chama cha ushirika; ukinunua kahawa kwa mkulima tukakujua kazi yetu ni kukufilisi.” Alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan John Bahama.

Mkurugenzi huyo alikuwa akiongea na wanakijiji wa Chivu, kata ya Kirushya Julai 30, 2018, baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema, kwamba Ndugu Rafaeli Festo Nfizi anavuna kahawa ya wakulima kinyume na utaratibu uliowekwa na serikali.

Ndugu Rafaeli alikuwa amekwisha vuna gunia zipatazo kumi na moja kwa shilingi 40,000/= tu, kitendo ambacho Mkurugenzi Mtendaji alikitaja kuwa ni cha kinyonyaji na cha kuwanyanyasa wananchi wa kawaida.

Baada ya kupata taarifa kwamba Mkurugenzi na timu yake, wanakwenda nyumbani kwa Ndugu Rafaeli, alikimbia; timu ilikuta gunia kumi na moja za kahawa alizokuwa amevuna kwa  wakulima.

Akiongea na wananchi wa kijiji cha Chivu, amesema chama cha ushirika cha Ngara Farmers Corporative mwaka 2018, kimepewa dhamana ya kukusanya kahawa yote ya wakulima wilayani Ngara.

“Kwa sababu Ndugu Rafael amekiuka utaratibu uliowekwa na serikali na kwa makusudi akamua kuendelea kufanya ufisadi wake, tutamfilisi kahawa yote, na itakuwa mali ya serikali.” Alisema Mkurugenzi Mtendaji Ndugu Bahama.

Ndugu Bahama amewaambia wananchi hao kufikisha ujumbe huo kwa wengine kwamba Kama kuna mtu alinunua kahawa ikiwa shambani asubiri mkulima aiuze, ili baada ya kuuza amlipe mlangunzi pesa yake; lakini mlanguzi hana ruhusa ya kuvuna kahawa ya mkulima.

Wakati huo huo, katika kjiji cha Mwivuza kata ya Kirushya timu hiyo ya Mkurugenzi ilimkamata Mwenyekiti wa Kitongoji cha Murugalama ‘A’ kijiji cha Mwivuza kata ya Kirushya, Ndugu Alani Jason, akituhumiwa kupokea kiasi cha shilingi 30,000/= kutoka kwa Sifa ili amruhusu mlanguzi kuvuna kahawa kwa wakulima.

Timu ilifanikiwa kukamata gunia nane toka kwa mkulima aliyekuwa ametunza kahawa za mlanguzi aliyejulikana kwa jina moja la Sifa wa kitongoji cha Lunzenze kata ya Ntobeye, nakufikisha jumla ya gunia zilizokamatwa 19.

 Mkurugenzi Mtendaji huyo wa Halmashauri ametoa wito kwamba waende wawaambie na wengine wasijaribu kuchukua kahawa ya mtu na wala wasijaribu kununua kahawa kwa mkulima yoyote.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NGARA YAFANYA VIZURI MICHEZO YA SHULE ZA MSINGI UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA

    May 30, 2025
  • MHE. COL MATHIAS KAHABI DC NGARA AKUTANA NA BALOZI WA RWANDA.

    May 29, 2025
  • NGARA YAENDELEA VIZURI NA MICHEZO YA SHULE ZA MSINGI UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA.

    May 26, 2025
  • MADEREVA WAPATIWA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI ILI KUPUNGUZA AJALI - NGARA

    May 24, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa