• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Upepo Waezua Madarasa Manne Wanafunzi Wapatao 400 Watakosa Mahali pa Kusomea

Wakati ilipowekwa: October 5th, 2018

Wanafunzi wapatao mia nne (400) wa shule ya msingi Rusumo kata ya Murukulazo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, watakosa mahali pa kusomea baada ya madarasa manne kuezuliwa na upepo kwa wakati tofauti.

Taarifa hizo ni kwa mujibu wa mkuu wa Kaimu Mkurugezi Mtendaji na Afisaelimu Msingi  Ndugu Gidion Samson Mwesiga  alipoongea na Tovuti ya Halmashauri Oktoba 04, 2018; kwamba madarasa yaliyoezuliwa ni ya wanafunzi wa darasa la kwanza, la pili na la tatu.

“Siku chache zilizopita madarasa mawili yaliezuliwa na kupelekea wanafunzi wapatao mia mbili (200) kusomea chini ya miti; sasa madarasa mengine mawili yameezuliwa wanafunzi wengine watakosa mahali pa kusomea.” Alisema Kaimu Mkurugenzi Mtendaji.

Kaimu Mkurugenzi huyo amesema upepo huo umetokea majira ya saa 8 mchana wakati wanafunzi wa darasa la nne walipokuwa wakifanya mitihani ya utimilifu ngazi ya mkoa, ambapo kila darasa lilikuwa na idadi yawanafunzi wapatao arobaini na wawili (42).

Alipoulizwa kama kulikuwa na madhara zaidi ya kuezuliwa kwa madarasa hayo; Kaimu Mkurugenzi alisema wanamshukuru Mungu kwani wanafunzi wote wako salama na hakuna madhara yoyote zaidi ya kuezuliwa kwa madarasa.

Amesema shule yake ni kama haipo kwani hata madarasa matatu yaliyobaki yaliwahi kuezuliwa, na kudai kwamba yanahitaji marekebisho makubwa; “kwa kifupi shule yangu haina miundo mbinu.” alisisitiza.

ili kuepuka madhara mengine ya aina hiyo, Kaimu Mkurugenzi ameagiza walimu wakuu na wakuu wa shule zote za msingi na za sekondari katika Halmashauri yaWilaya ya Ngara kupanda miti katika msimu huu wa mvua unaoanza hivi karibuni.

wakati Halmashauri inajipanga kufanya ukarabati wa madarasa hayo Kaimu Mkurugenzi amnewataka watendaji wa kijiji na kata wa kuitisha mkutano wa hadhara ili kujadili na kuona namna ya kurekebisha majengo hayo ili watoto wapate mahali pa kusomea kabla ya mvua kuanza.

Wakati huo huo, Mratibu wa Maafa Wilaya ambaye pia ni Afisa Mazingira wa Wilaya hiyo Ndugu Waziri Zawadi amewataka wananchi wilayani Ngara kupanda miti katika maeneo yao, ili kuepusha majanga ya upepo na kuongeza kwamba watu wanatabia ya kukata miti na kusahau kupanda mingine.

“Tukiendelea na tabia ya kuharibu mazingira hatutakuwa na njia rahisi ya kukwepa majanga kama haya, hata hivyo ni kumshukuru Mungu kwamba hakuna kijana aliyepoteza maisha katika tukio hili.” alisema mratibu huyo wa Maafa Wilaya.

Shule ya Msingi Rusumo ina wanafunzi zaidi ya mia saba (700), ambapo karibu nusu ya wanafunzi hao, hawana mahali pa kusomea kufutoa janga la upepo mkali ulioezua madarasa manne (04) kwa wakati tofauti.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa