• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Waelimisheni Wananchi Vijijini Kuhusu Athari za Ugonjwa wa Ebola, Lt. Col. Mntenjele

Wakati ilipowekwa: January 10th, 2019

Wahamasishaji na watoa elimu kwa wananchi kuhusu athari za ugonjwa wa Ebola katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, wametakiwa kwenda kutoa elimu hiyo vijijini kwani wananchi hao bado hawana uelewa wa ugonjwa huu, ikilinganishwa na wale wa mjini.

Mkuu wa Wilaya ya Ngara, ambaye ni mwenyekiti wa kikao cha kikosikazi cha Kupambana na Ugonjwa wa Ebola wilayani Ngara Lt. Col. Michael Mntenjele, ametoa wito huo wakati wa kikao cha kuweka mikakati ya jinsi ya kudhibiti ugonjwa huo wilayani humo.

Kikaokazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Mkuu waWilaya Januari 09, 2019; kiliwahusisha wafanyakazi wa idara ya afya, taasisi zote za umma na za binafsi, wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri, waandishi wa habari na vyombo vya ulinzi na usalama wilayani humo.

“Wananchi wa mjini wana nafasi ya kupata elimu ya Ebola kupitia matangazo mbalimbali, lakini wananchi wa vijijini hawana nafasi hiyo, nashauri waelimishaji mwende vijijini, tumieni siku za soko wanapokuwa wamakusanyika; wafundisheni juu ya athari za ugonjwa huu hatari.” Alisema Lt. Col. Mntenjele.

Amesema kumekuwepo na mazoea ya kuwaelimisha viongozi; watendaji, madiwani na wenyeviti wa vijiji kwa matumaini kuwa watasambazi elimu waliyopata kwa wananchi, lakini uzoefu umeonyesha, wakishapata mafunzo hayo, hawayapeleki kwa wananchi.

Amewataka wataalamu kutoka mkoani na hata Wizarani watembelea maeneo ya vijijini, ambako kuna njia zisizo rasmi, zinazotumiwa na wananchi kutoka nchi jirani kuingia hapa nchini, kuliko kutembelea mipaka ya Rusumo na Kabanga.

“Kukitokea tatizo katika mojawapo ya nchi jirani hakuna mkimbizi au mhamiaji haramu atakayepita kwenye ‘scanner’ tulizoweka Rusumo na Kabanga; bali watatafuta njia iliyorahisi kwao kuingia nchini kwetu; hivyo, tujikite katika njia zisizo rasmi.” Alisema Lt. Col. Mntenjele.

Akitoa mfano, amesema wageni wanaopima ni wale wenye hati na kazi rasmi za kuja kufanya hapa nchini, lakini imedhihirika kuwa watu wa bodaboda wanapita tu bila kupima, huku akionya kuwa kwa mtindo huo wilaya ya Ngara iko katika hatari zaidi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halamashauri ya Wilaya ya Ngara Ndugu Aidan Bahama, amezitaka kamati zilizoundwa kupambana na ugonjwa wa Ebola wilayani ngara, kuwajibika ipasavyo, ili kudhibiti ugonjwa huo, huku akionyesha wasiwasi wa kutokuwa na vitendea kazi vya kudhibiti ugonjwa huo.

“Nasikitika kwamba Wilayani kwetu hatuna vifaa vya kutosha kudhibiti ugonjwa huu; mbaya zaidi, vifaa vinavyotakiwa ni vya gharama kubwa, ambavyo Halmashauri yetu haina uwezo wa kuvinunua, kwani hata magari ya wagonjwa tuliyonayo; hayafai kuwasafirisha wagonjwa wa Ebola.” Alisema Ndugu Bahama.

Akatoa wito iandikwe barua ya kuomba vitendea kazi toka ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera Dr. Marco Mbata, ili vituo vya afya vilivyoko katika vijijiji vya mpakani, viweze kupata ‘toolkit’ mbili au tatu za kutibia wagonjwa wa Ebola kwa kila kituo ikiwa watapatikana.

Naye Katibu Tawala wa Wilaya ya Ngara Ndugu Vedastus Tibaijuka, ametoa angalizo kwa vyombo vya habari kutotoa taarifa za kusikia mtaani, badala yake wawasiliane na uongozi wa Wilaya ya Ngara, kwani kwa kufanya hivyo watatangaza habari za uhakika.

Amezitaka kamati kufanyakazi kama timu, kwani ugonjwa wa Ebola hauwahusu wafanyakazi wa afya tu, bali ni ugonjwa mtambuka unaozihusisha idara na vitengo vyote hapo wilayani; huku akionya kuachana na mila na desturi katika kupambana na ugonjwa huu, hasa katika suala la mazishi.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa