• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Wakazi wa Kibogora wahaswa kusambaza Elimu ya Athari za Mabomu.

Wakati ilipowekwa: February 14th, 2018

Kaimu Mkurugenzi wa wilaya ya Ngara Gideon Mwesiga amewahasa wanasemina kuwaelimisha wananchi katani Kibogora kuhusu athari za mabomu ili waweze kuwatuliza kisaikolojia. Ameongeza kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kujikubali na hivo kuendelea na maisha yao ya kawaida.

Ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya msaada wa kisaikolojia kwa wahanga wa mlipuko wa bomu katika shule ya msingi Kihinga mwishoni mwa mwaka jana. Mafunzo hayo yanafanyika katika shule ya sekondari ya Kibogora katika kata ya Kibogora.

Mafunzo hayo yatakayodumu kwa siku tano yanaratibiwa na shirika la Jambo Bukoba. Mafunzo  yanawajumuisha Diwani wa kata ya Kibogora Mh. Adroniz E. Burindoli, wazazi, wakuu wa shule za msingi, maafisa Elimu Kata wa kata za Bukiriro na Kibogora, watoto 30 kutoka katika shule za msingi  Kihinga, Nyarukubala na Nyarulama pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Kibogora.

Katika mafunzo hayo mada zinazofundishwa ni ullinzi na usalama kwa watoto, malezi na msaada wa kisaikolojia, mafunzo juu ya hisia, uwezo wa kurejea katika hali ya kawaida na namna ya kujikinga na mabomu.

Amesema mafunzo hayo yatakuwa na maana na kutimiza lengo lake ikiwa waliohudhuria watawashirikisha wananchi wenzao ambao hawakupata mafunzo hayo kile walichojifunza, vinginevyo yatakuwa hayana maana.

Akisistiza alisema kuwa, kama watawashirikisha wenzao watakuwa wamewasha taa iwamulikie wote, kinyume chake watakuwa wamewasha taa na kuiweka chini ya uvungu wa kitanda.

Aidha alitumia nafasi hiyo kuwashukuru baadhi ya wadau waliotoa misaada ya hali na mali kuhakikisha kuwa waathirika wanapata matibabu na mafunzo ya kisaikolojia, kuwa ni Jambo Bukoba, Chama cha Walimu, Tumain Fund, Caritas, wafanyabiashara, na wanajeshi wa jeshi la wananchi wa Tanzania.

Alisema kuwa Halmashauri imetenga jumla ya shilingi milioni tisa kwa ajili ya kulipia gharama za matibabu za wahanga wa bomu waliotibiwa katika hopitali ya Kagondo na wale watakaokwenda kutibiwa KMC Moshi.

Naye Meneja wa Jambo Bukoba Ndg. Gonzaga Stephan amesisitiza kuwa wanaweza kufanya kazi katika mazingira salama kama hakuna hofu ya ulipukaji wa mabomu. Aidha ameongeza kuwa mtoto anapoathirika hata Jambo Bukoba inaathirika, ndiyo maana wanaratibu mafunzo haya ili kunyumbulisha maisha ya watoto ili warejee katika hali yao ya kawaida.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa