• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Watumieni Dada Zenu Mfanye Vizuri Katika Mitihani

Wakati ilipowekwa: April 17th, 2019

Wanafunzi wa O-Level katika shule ya sekondari ya Muyenzi, wametakiwa kuwatumia wanafunzi wa A-Level, ili wawasaidia katika masomo yao, wafanye vizuri katika mithani ya ndani na ya taifa.

Akiongea na wanafunzi Aprili 12, 2019 wakati wa mahafali ya wanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Muyenzi Afisaelimu Idara ya Sekondari Ndugu Fikeni Ezekiel Senzighe amesema kuanzishwa kwa tahsusi za sanaa na sayansi ni neema kwani watoto watafanyavizuri ikiwa watawatumia dada zao.

“Shule nyingi zinazokuwa na kidato cha tano na cha sita wanafunzi wa vidato vya chini wanafanya vizuri; kwa hiyo tunatarajia kwamba katika masomo ya Arts shule hii itafanya vizuri zaidi kwani dada zao watawasaidia.” Alisema Ndugu Fikeni.

Amewaambia washereheka kwamba shule ya ya sekondari Muyenzi imeongeza tahsusi za masomo ya sayansi, abapo kwa kuanza itakuwa na tahsusi ya CBG Chemistry, Biology na Geography, kwa hiyo kidato cha tano wataoingia mwezi Julai 2019 watasoma masomo ya sayansi.

Akijibu itawezekanaje wakati shule hiyo ilikuwa na mchepua wa sanaa, Afisaelimu huyo amesema shule ina maabara za kutosha zilizosheheni vifaa vya sayansi vya kutoshereza mahitaji kwa wanafunzi watakaosoma tahsusi ya CBG.

“Kukua kwa shule hii kitahsusi ni chachu katika kufanya vizuri zaidi hapo baadae kwani watakuwa msaada mkubwa kwa wadogo zao; kwa hiyo, vijana wa O-Level watumieni dada zenu wa A-Level pale mtakapokwama katika masomo yenu, ili wawasaidie.” Ndugu Senzighe.

Aidha, amewashukuru wazazi na uongozi wa Kata ya Rulenge kwa kuanzisha utaratibu wa wanafunzi kupata uji shuleni akidai kwamba mtoto anapokuwa ameshiba anakuwa na utulivu wa fikirana na utayari wa kupokea kile anachojifunza.

“Nimefarijika kusikia kwamba wanafunzi walau wanapata uji mwanafunzi anapopata chakula cha mchana au angalau uji anapata nguvu ya kuweza kuendelea na masomo yake; na anakuwa na nguvu ya kuweza kujifunza zaidi, lakini pia kunakuwa na amani darasani.” Ndugu Senzighe.

Katika risala zilizosomwa nyingi zimeonyesha changamoto ambazo zinaikabili shule hiyo, ambazo ni pamoja na upungufu wa madarasa, madawati, matundu ya vyoo, ukosefu wa umeme na upungufu wa walimu.

Amesema kwamba katika sekta ya elimu mapungufu yapo na yako katika mawanda waliyoyataja, serikali inayafahamu na inaweka utaratibu ambao utayamaliza hatua kwa hatua, hata hivyo wakati serikali inajipanga kutatua changamoto muendelee kusoma kwa bidii ili muweze kufanya vizuri katika mitihani yenu.

Shule ya sekondari ya Muyenzi ilifanya mahafali ya sita ambapo wanafunzi wapatao 64 wanatarajia kufanya mtihani wa kuihitimu kidato cha sita Mei 06, 2019, huku wakitakiwa kuendelea kuwa na nidhamu na kusoma kwa bidii ili waweze kupata kile kilichowaleta shuleni hapo.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • DC NGARA MHE COL MATHIAS KAHABI AKUTANA NA BRIG GEN GABRIEL E. KWILIGWA - KAMANDA BRIGDE YA MAGHARIBI.

    May 16, 2025
  • MHE COL MATHIAS JULIUS KAHABI DC NGARA ASHIRIKI USAFI NA WANANCHI WA NAKATUNGA

    May 15, 2025
  • MWENYEKITI WA CCM AENDELEA NA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO - NGARA

    May 16, 2025
  • KIKAO KAZI CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA AFUA ZA LISHE WA KILIMO CHA MAHINDI CHAFANYIKA - NGARA

    May 16, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa