• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Ngara District Council
Ngara District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya wilaya ya Ngara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Mipango na Ufuatiliaji wa Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu
        • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya sekondari
        • Kwa wanafunzi
          • Mitihani iliyopita
            • Kidato cha IV
      • Maji
        • Maji Mjini
        • Maji Vijijini
      • Kilimo, umwagiliaji na ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi na zimamoto
      • Usafi na Mazingira
    • MSM
      • Huduma katika MSM
      • Muundo wa MSM
    • Kata
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za kisheria
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili ya Msingi
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
      • Mipango Miji na Mazingira
    • Ratiba
      • Vikao vya waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Nyumba ya Picha

Wizara ya Maji Haitatoa Ushirikiano kwa Wahandisi Wababaishaji; Mh. Aweso

Wakati ilipowekwa: January 13th, 2019

“Wahandisi ambao wana uwezo wa kufanyakazi tutawapa ushirikiano, wahandisi wababaishaji hawana nafasi ya kufanyakazi katika wakala wa maji vijijini; kwa sababu tumejipanga kuhakikisha adhima yetu ya kumtoa mwanamama ndoo kichwani inakamilika.” Alisema Naibu Waziri wa Maji Mh. Jumaa Hamidu Aweso.

Naibu waziri wa Maji Mh. Aweso ameyasema hayo Januari 13, 2019 katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, wakati wa ziara yake ya siku moja Wilayani humo, ambapo amesema waliagizwa kuhakikisha watanzania wanapata maji safi, salama na yenye kutoshereza.

Maji hayapatikani kwa kukaa ofisini na kuzunguka kwenye kiti cha kuzunguka; maji yanapatikana kwa wataalamu kwenda vijiijini kuona maedeleo ya miradi ya maji inavyotekelezwa, na inapokwama hasa changamoto zinazowakabiri wananchi.” Alisema Mh. Aweso

Zipo jitiada zinazofanywa na serikali kutatua matatizo ya upatikanaji wa maji; kwa mfano, Bukoba kuna mradi mkubwa ambao serikali imewekeza zaidi ya shilingi milioni 31; lakini yapo maeneo ya pembezoni hayana maji kama Ihungo.

Amsema Wizara inatoa nguvu kwa Manispaa ya Mji wa Bukoba, ili kuhakikisha kwamba maeneo ya pembezoni nayo, yanapata maji, ili wananchi wa mjini humo waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Kubwa alilogundua katika Mkoa wa Kagera ipo miradi mikubwa imekamilika, lakini haitoi maji; mingine iliyokamilika matenki yanavujua na imetelekezwa na wakandarasi wamelipwa fedha lakini wananchi hawapati huduma ya maji.

“Unamlipaje mkandarasi kazi hajaifanya vizuri, na hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa dhidi yake; sisi kama wizara ya maji hakuna mhandisi yeyote, ambaye ataaribu miradi ya maji halafu ategemee sisi tutamhamisha; tutamchukulia hatua na kama ameshiriki na wakandarasi kula fedha za serikali ajiandae kuzitapika.” Alisistiza Waziri Aweso.

Kwa hiyo Wizara imeanzisha wakala wa maji vijijini na mswada umeishasomwa bungeni, ambao baadae wanatarajia uatapita Bungeni ili uwe sheria kusidi Wizara iweze kuchukua hatua stahiki kwa wabadhirifu wa miradi ya maji.

Amesema kabla hao wahandisi wa maji hawajanza kufanya kazi na wakala wa huduma ya maji vijijini, watapigwa msasa kwa sababu watakaosimamia wakala huu ni hao hao waandisi, ambao wanatoka katika Halmashauri za wilaya.

Amekiri kuwepo kwa changamoto ya ucheleweshaji wa fedha za miradi, na kuahidi kuyalipa madeni ya wakandarasi wa maji hapa Wilayani Ngara; ambapo kiasi wanachodai amekitaja kuwa ni kama shilingi milioni 231,000,000

Naye Kaimu Mhandisi wa Maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara Eng. Simon Ndymukama amekiri kuwa Mji wa Ngara una upungufu mkubwa wa maji kwa sababu ya changamoto tau meme na ongezeko la watu.

“Ni kweli maji yanapatikana kwa mgao; ambapo maeneo mengine wanapata maji mara mbili kwa wiki; lakini wengine inaweza ikawa mara moja kwa wiki, tatizo kubwa  ni changamoto ya umeme, kwani ni mdogo kuweza kuendesha mitambo ya kusukuma maji.” Alisema Eng. Ndyamukama.

Pia maji yanayozalishwa ni kidogo ikilinganishwa na uhalisia na kudai kwamba mfumo wa maji uliopo umejengwa mwaka 1972 na ongezeko linakuwa wahitaji huduma eneo la mjini; huku miundombinu ni ile ile.

Hata hivyo, amesema kuna mradi mkubwa wa miji sita ambapo Ngara ni miongoni mwa wilaya zitakazinufaika na mradi huo, na uko katika hatua za mwisho za kuanza; utakapokamilika tatizo la maji katika mji wa Ngara utakuwa ndo mwisho wake.

Matangazo

  • RATIBA YA MKUU WA WILAYA YA NGARA MHE COL MATHIAS J KAHABI TAREHE 18/11/2024 MPAKA TAREHE 24/11/2024 November 18, 2024
  • TANGAZO LA WITO KWA WATUMISHI WA UMMA WALIOOMBA KUWAFUATA WENZA WAO November 19, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA WILAYANI NGARA KWENYE TARAFA ZA MURUSAGAMBA NA RULENGE November 22, 2024
  • SEMINA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA WASIMAMIZI WA VITUO IMEFANYIKA TARAFA ZA KANAZI NA NYAMIAGA November 24, 2024
  • Tazama zote

Habari mpya kabisa

  • NGARA YAFANYA VIZURI MICHEZO YA SHULE ZA MSINGI UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA

    May 30, 2025
  • MHE. COL MATHIAS KAHABI DC NGARA AKUTANA NA BALOZI WA RWANDA.

    May 29, 2025
  • NGARA YAENDELEA VIZURI NA MICHEZO YA SHULE ZA MSINGI UMITASHUMTA NGAZI YA MKOA.

    May 26, 2025
  • MADEREVA WAPATIWA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI ILI KUPUNGUZA AJALI - NGARA

    May 24, 2025
  • Tazama zote

Video

ZIARA YA KAMATI ZA BUNGE KUTEMBELEA TEMBO NICKEL WILAYANI NGARA KAGERA
Video za ziada

Kurasa za haraka

  • Reports
  • Acts
  • Application form
  • Organization Structure
  • E-MREJESHO

Kurasa mashuhuri

  • PSM (Public Service Management)
  • PO-RALG
  • NECTA
  • NACTE
  • Sekretarieti ya ajira
  • Mfumo wa kutuma,kupokea na kufuatilia malalamiko,mapendekezo,maulizo na pongeza(eMalalamiko)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo la Ngara

Wasiliana nasi

    Ngara District Council

    Anuani ya Posta: P.O.Box 30, Ngara

    Simu ya mezani: 0282226016

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: ded@ngaradc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimilki ©2017 Halmashauri ya wilaya ya Ngara. Haki zote zimehifadhiwa